About KABENDE.COM

Manual Description Here: Ea eam labores imperdiet, apeirian democritum ei nam, doming neglegentur ad vis.

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU 38 NA 39

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 38 & 39
MTUNZI:Enea Faidy
.....Mr Aloyce bado hakumuelewa vizuri mkewe kwa kauli aliyoisema. Kauli ile iliibua utata mkubwa kichwani mwake na kumtaka mkewe amueleze ukweli.
"Niambie mke wangu... Nini kinaendelea? Maana Mimi sielewi!" Alisema Mr Aloyce kwa sauti ya upole ili mkewe amweleze ukweli wote. Lakini kwa bahati mbaya sana Maimuna alisita kueleza ukweli ambao alitaka kumwambia Mr Aloyce.
Viboko mfululizo vilivyosikika kwa sauti kubwa vilimshukia Maimuna na kumfanya ahangaike kupita kupita kiasi. Aligalagala pale chini kama nyoka aliyepondwapondwa kichwa chake. Sauti na yowe la kilio viliibuka kwa Maimuna kwani alishindwa kuvumilia maumivi ya viboko alivyochapwa na MTU asimfahamu.
"Nasemaaa!nasemaaa!" Alisema Maimuna huku akilia.
Mr Aloyce na Mlinzi wake walibaki na mshangao kwani kila walichokiona walihisi ni muujiza tu. Walibaki kimya huku wakimshangaa mwanamke yule.
"Aloyce... Mimi ni mchawiiii.." Alisikika Maimuna na kwa bahati mbaya sana alishindwa kuongea kwa sauti ndogo hivyo sauti ilipaa sana na kuwafanya wapita njia na majirani kujazana sana nje ya geti kwa Mr Aloyce. Kwa uzito wa adhabu alioipata Maimuna ilimbidi tu aseme ukweli wote uliomwacha mdomo wazi Mr Aloyce.
"Naitwa Maimuna.. Sio mama yake Eddy kama ulivyodhani..." Alisema Maimuna na kumfanya Aloyce ahamaki. Alichanganyikiwa sana na kushindwa kuzungumza.
"Nisamehe Aloyce... Nilikuja kuiteketeza familia yako.... Mkeo alishaliwa nyama ... Mimi nilikuja kumlinda Eddy ili sehemu zake za siri zibaki mikononi mwa Doreen"
"What? Ati nini? Kwanza Doreen ni nani?" Mr Aloyce alijikuta anauliza maswali matatu mfululizo huku hasira zikiwa zimempanda kupita kiasi. Alitamani achukue jiwe zito na kumponda nalo mwanamke yule.
"Ni mchawi... Alikuwa anasoma na Eddy..." Alisema Maimuna huku akilia kwa sauti kubwa.
"Oh! Shit!" Alisikika baba Eddy.
Watu waliokuwa pale nje walizidi kutafuta upenyo wa kuingia mle ndani. Lakini geti lilikuwa limefungwa, kelele nyingi kutoka nje zilizidi kusikika.
"Mchawiiiiii! Mchawiii! Tufungulie tumwadhibu huyo mchawiiii!! Funguaa! Mwanamke mchawi hafai kuishi!!" Sauti zile kutoka nje zilimhamasisha mlinzi kufungua geti na kuwaruhusu watu waingie. Cha ajabu watu wale waliingia wakiwa wameshikilia silaha za aina mbalimbali. Wengine mawe wengine visu huku wengine wakiwa wameshikilia fimbo na mapanga. Hali ilichafuka sana pale ndani.
Umati wa watu ulikuwa uvamia uwanja wa Mr Aloyce tayari kwa kumwadhibu mchawi aliyesababisha kilio na majonzi katika familia ya ile iliyokuwa imejaa upendo na amani hapo awali."Tuue tu... Afe Huyo" walisema. Ghafla Maimuna akabadilika na kuwa kiumbe tofauti na vile anavyofahamika wote wakashtuka.
*****
Doreen aliendelea kushangaa kwa hofu sana ndani ya chumba kile. Upepo mkali uliovuma chumbani mle na kuangusha baadhi ya vitu vilivyokuwa vimewekwa vizuri ulimfanya Doreen ajione mdogo kama sisimizi juu ya janga lile.
Akiwa bado haelewi la kufanya ghafla sura ya MTU aliyemfahamu ikatokea mbele yake na kumfanya Doreen apigwe na mshangao wa hali ya juu.
"Haa! Dorice!" Alisikika Doreen akiita kwa mshangao.
"Mimi hapa! Sema nikusikie!" Alisema Dorice kwa sauti iliyojaa dharau kupita kiasi. Kisha kabla hajaendelea na lolote akanyoosha kidole chake ukutani na ghafla kikatokea kama runinga pana iliyoonesha siku ambayo Doreen alimpaka kamasi usoni kiuchawi ili asipendwe na Eddy. Kisha akaonekana Doreen akimkata Eddy sehemu zake za siri.
"Ulikuwa mjanja sana sio?" Alisema Dorice. Doreen hakuamini macho yake alitetemeka kwa hofu kupita maelezo.
"Do..Dor...Dorice... Umepata wapi huo ujasiri wa kunitisha kiasi hicho?" Aliongea Doreen kwa kigugumizi sana. Dorice alimtazama Doreen na kucheka kidogo huku akitembeatembea ndani ya chumba kile.
"Ulininyang'anya penzi langu kinguvu kwa mtu nimpendae sana.. Cha ajabu ulitaka kumharibia yeye na familia yake... Kwanini wewe in katili na mbaya kitabia kuliko sura yako?" Aliuliza Dorice.
"Tafa..Tafadhali Dorice nisamehe.."
"Nimekusamehe tangu zamani... Ila nataka kukufunza adabu. Umeua wengi sana wasiokuwa na hatia umewaharibu wengi sana bila kosa." Alisema Dorice na kutoweka machoni mwa Doreen.
Doreen alichanganyikiwa mno, lakini kilia alipotaka kupotea na kumtoroka Dorice hakuwa na nguvu, kwani Dorice alikuwa na nguvu nyingi mno ambazo zilimsaidia kufanya kila alichokitaka. Na hakuna mchawi ambaye angeweza kumshinda Dorice kwa wakati ule.
Ghafla bin vuu! Kichapo kikali kikamshukia Doreen. Alihisi mawe mazito yanamshukia kichwani mwake na kumpiga kwa nguvu. Alihisi maumivu makali mno. Akapiga ukunga mkali baada ya kushindwa kuvumilia maumivu Yale. Hakuona sababu ya yeye kuendelea kukaa ndani ya chumba kile huku akitaabika akaamua kufungua mlango na kutoka nje ya chumba huku akilia kwa sauti kali . kilio chake kiliwashtua wengi na kuwafanya watoke njee kutazama kulikoni.
Umati wa watu ulifurika kumtazama Doreen pale nje. Alikuwa uchi wa mnyama huku akipiga kelele sana.
"Naacha uchawiii... Mimi si mchawi...uwiiiii... Nisaidieni" alilalama huku akipiga mbio bila kujali kuwa hajavaa nguo yoyote.
Watu walianza kumfuata huku wakipiga kelele "mchawii! Mchawiiii" "masikini we! Binti mzuri hivi kumbe ana mambo ya uchawi?" Walisikika watu wakiongea vikundi vikundi.
Watu walikazana kupiga picha huku wengine wakiokotw mawe na kumfukuza Doreen huku wakimtupia mawe.
Doreen alikimbia sana huku akipiga kelele sana.
Ghafla mama mmoja alipiga kelele sana
"Huyu mtoto aliinibia pesa zangu mgahawani kumbe ni mchawi! Alaaniwe!"
"Mimi alikuja dukani kwangu akataka aniwangie Leo ameumbuka" walizungumza yule mama wa mgahawa ambaye alitapeliwa na Doreen kwa mazingira ya kutatanisha sana ndipo alipojibiwa na mwanaume mwingine ambaye Doreen alijaribu kumuwangia ili aibe pesa.
Doreen alizidi kupiga mbio sana huku umati ule wa watu mjini Iringa ukizidi kumfata kwa kasi wakiwa wameshika mawe na wengine viboko.
*****
Baba Pamela alikuwa ametulia kidogo huku akimtazama binti yake kwa masikitiko makubwa.
"Daddy najisikia hasira hata kumtazama mama" alisema Pamela huku akilia.
"Hutakiwi kuwa hivyo... Nataka tufanye jambo hapa!"
"Jambo gani mume wangu?" Aliuliza mama Pamela.
"Nataka tumwombe Mungu mpaka atujibu juu ya binti yetu"
"Hakuna tatizo mume wangu.." Alisema mama Pamela kwani tayari maneno ya mumewe yalimpa nguvu hata ya kuzungumza.
"Pamela una amini kama Mungu anaweza kutenda mambo ambayo sisi hatuwezi?"
"Ndio naamini... Lakini..."alisema pamela
"Lakini nini? Ukiwa na imani hutakiwi kutilia shaka.."
"Sawa baba niombee tu.."
Baba Pamela aliwataka wote wapige magoti kisha wakaanza na nyimbo na baada ya hapo akaanza kufanya maombi. Aliomba sana akiwa anataka Mungu amrudushie mwanae titi lake.
Radi Kali zikaanza kupiga katika nyumba zilipiga radi nyingi wakati baba Pamela akiendelea kusali kwa bidii na imani sana. Ghafla akawaambia watoke nje wote.
"Roho wa Mungu ananiambia kuna kitu kimefukiwa pale nje ili kutuangamiza" alisema baba Pamela kisha wote wakatoka nje. Baba Pamela aliongoza njia mpaka Pale ambapo Mama Pamela alifukia sahani iliyokuwa na kinyesi. Wakafukua.
Cha ajabu akatokea nyoka mkubwa sana ambaye hakuna aliyetarijia kama angekuwa pale.
"Mungu wangu!" Alisikika Mama Pamela akizungumza kwa woga. Baba Pamela alizidi kumwomba Mungu mpaka yule nyoka alipobadilika na kuwa na sura ya Doreen lakini mkiani akabaki kuwa nyoka. Wote walistaajabu sana huku wakitetemeka kwa woga...
RIWAYA:MWANAFUNZI MCHAWI - SEHEMU YA 39
...."Ina maana Doreen ni mchawi kiasi hiki?" Alijikuta anaropoka kwa mshangao mama Pamela. Pamela alizidi kushangaa huku akimtazama mama yake kwa mshangao kisha akimtazama chatu yule mwenye sura ya Doreen. Baba Pamela aliendelea na maombezi yake kwa imani kali. Yule chatu alijigeuza geuza kwa vitisho vikali sana huku akijaribu kupambana Na Baba Pamela kwa kujitoa kwenye lile shimo dogo.
Lakini kwa bahati njema chatu yule alipigwa na radi Kali sana iliyoharibu uso wake na kuweka mipasukopasuko iliyoacha damu ichuruzike kirahisi. Baba Pamela hakuacha kuomba na kuithibitisha imani yake thabiti. Ghafla ukatoka moshi mkali kutoka kwenye mdomo wa sura ya Doreen iliyopo kwa yule chatu.
Moshi ule ulikuwa wa ajabu sana Kwani ulikuwa katika mstari ulionyooka mpaka kifuani kwa Pamela, na hata Pamela alipojaribu kukimbia moshi ule ulimfuata kila alipoenda na kumfanya Pamela aogope zaidi. Pamela alipoona hawezi kuukwepa moshi ule akasimama wima akisubiri kuona kitakachotokea huku akihema nguvu sana.
Moshi ule ulitua taratibu kifuani kwa Pamela kisha ule mstari uliokuwa umejitengeneza ukapotelea kifuani kwa Pamela taratibu sana. Pamela alijishangaa sana Kwani alihisi mabadiliko Fulani mwilini mwake. Alitulia kimya huku akimtazama baba yake.
Baba Pamela alipohitimisha maombi yake yule chatu alipigwa radi Kali kisha akatoweka machoni kwa wanafamilia wale.
"Jina la Bwana lihimidiwe kwani ametenda tulichokitaka.. Amejidhihirisha mbele yetu.. Oh asante Bwana wa Majeshi" alisikika baba Pamela huku akiinua macho yake na mikono yake juu ili kumshukuru Mungu kwa ajili ya maombi yake.
"Pamela hebu jitazame kifuani kwako" alisema Baba Pamela huku akitabasamu na kutoa kitambaa laini mfukoni na kujifuta jasho lililokuwa limetapakaa usoni kwake kama chemchem ya maji.
Mama Pamela alimsogelea mwanae na kumsaidia kushuhudia kilichotokea kifuani kwake. Walisogea pembeni kidogo, kisha Pamela akajifunua shati lake na kujitazama kwa umakini. Wote hawakuamini kilichotokea kwani titi lake lilikuwa limerudi kama lilivyokuwa. Pamela alishtuka sana na kupiga kelele za shangwe huku akiruka kama ndama. Akamkimbilia baba yake na kumkumbatia kwa nguvu.
"Baba! Nashukuru baba! Asante!" Alisema Pamela kwa furaha kuzidi kiasi.
"No Pamela! Mshukuru Mungu sio mimi" alisema Baba Pamela huku akitabasamu.
Pamela alimuachia baba yake na kumfuata mama yake, chozi likamdondoka kwa uchungu huku akimkumbatia mama yake.
"Nisamehe sana mama! Naomba unisamehe kwa kukufanya ukose amani na kujisikia vibaya kwaajili yangu. Nakupenda sana mama.. Nisamehe mama!" Alisema Pamela huku akilia kwa uchungu.
"Pamela mwanangu! Usijali kwa yote yaliyotokea nilishakusamehe" alisema mama Pamela huku akimkumbatia kwa mahaba mazito binti yake mpenzi.
Baba Pamela alisimama pembeni yao kisha akapiga hatua za taratibu na kuwasogelea.
"Mke wangu... Familia yetu ingekuwa pabaya sana kwaajili ya yule adui! Lakini ni funzo kwako kuwa usimwamini kila mtu pia jifunze kumcha Mungu kwa moyo wote"
"Ashukuriwe Mungu sana! Tangu Leo wote tutamcha Mungu" alisema Mama Pamela.
"Kweli kabisa.. Mungu ni mkuu" alisema Pamela kisha Wote wakakumbatiana kwa furaha, ile furaha ya mwanzo ikawa maradufu. Kila mmoja alionekana kufurahi sana ule umoja uliotaka kuvurugika ukarejea tena katika familia ile ikazidi kung'ara na kuwa familia bora.
"Hakuna wa kumfananisha na Mungu!" Walisema kwa pamoja huku wakiwa na furaha ya ajabu.
*****
Leyla alipokea ugeni kutoka kanisani kwake ambapo wanamaombi watano walitia timu nyumbani kwake na kuiikuta familia ile ikiwa imepoteza furaha kabisa.
Leyla aliwakaribisha wageni wake vizuri na kuwakaribisha viti.
Mwalimu John na Judith walikuwa wapo kimya tu ingawa moyoni mwao walifurahia ujio wa watu wale.
Leyla akaamua kuwaambia kila kitu kilichotokea ndipo Walipoanza maombi yao. Walijtahidi kusali kwa imani kubwa sana. Baada ya maombi ya kama SAA zima ndipo maombi yao yalipoanza kujibiwa. Mambo ya ajabu yalianza kutokea ambApo mwalimu John alianza kuzungumza lakini cha ajabu funza walianza kutoka tena miguuni.
"Kuna mtu ni mchawi hapa" alisema Mwalimu John na kuwafanya wote wastaajabu.
"Tulia mume wangu watu wanakusaidia..." Alisema Leyla akimwambia mumewe.
"Nasema kuna Mtu anaroga hapa... Atoke.." Maneno hayo ya Mwalimu John yaliwafanya wote watazamane na kusitisha maombi kwa muda. Mwalimu John aliendelea kuongea.
"Wewe acha kuroga maombi ya wenzako... Wewe! Nikuseme?" Alisikika mwalimu John wakati huo wote walikuwa wameinamisha sura zao chini wakiogopa kutajwa. Baada ya dakika kadhaa kupita Mwalimu John alimsogelea mwanamke mmoja na kumshika bega.
"Sema ukweli la sivyo hawa funza wanahamia mwilini mwako.." Alisema mwalimu John huku akimkazia macho mwanamke yule.
"Mi..mimi..nime.. Mimi.." Alibabaika yule mwanamke.
"Ukidanganya tu funza wanakuhamia..."
"Ahm..aah.. Kweli.. Nilitaka..nilikuwa naroga msiendelee na maombi.." Alisema yule mwanamke akiwa anaona aibu kupita kiasi.
"Haya tokaa" aliamrisha mwalimu John na yule mwanamke akaondoka haraka huku kila mtu akimtazama kwa mshangao.
Hawakupoteza muda maombi yakaendelea na hawakutumia muda mrefu sana funza kwa mwalimu John wakapotea wote. Na mara ile Judith aliona ulimi wake ukiwa mwepesi sana na akaweza kuongea. Mwalimu John alikuwa kama aliyetoka usingizini alishtuka mno kuona kila kinachoendelea.
"Jamani.. Doreen ulitaka kuniua? Kwanini Doreen?" Alisema mwalimu John.
"Doreen ni nani?" Aliuliza mwanamaombi mmoja.
"Ni mwanafunzi wangu... Ni mchawi sana alitaka kuniua na alinifanyia mambo ya aibu sana" mwalimu John akasimulia kila kitu kuhusu Doreen.
Judithi pia akaeleza kila kitu kilichompata Mwalimu Jason ambaye tayari alishafariki dunia.
"Oh poleni sana watumishi Mungu ni mwema... Cha msingi mumrudie yeye!"
"Amen!"
Hatimaye mwalimu John na Judith wakarudia hali ya kawaida na furaha yao ikarejea tena. Walimshukuru sana Mungu.
Mwalimu John alimsogelea mkewe na kumbatia kwa dhati na upendo.
"Asante kwa upendo wako wa dhati uliokufanya uwe mvumilivu mno kwangu... Nakupenda!" Alisema mwalimu John na Leyla akatabasamu tu.
Wanamaombi wale walishukuru Mungu na kuwasihi familia ile pamoja na Judith kutomuacha Mungu. Kisha wakaondoka zao.
*****
Doreen alipokuwa anakimbia ndivyo kadri kipigo kilipomzidia. Kwani aliadhibiwa sana na Dorice na wakati huohuo Mungu alikmwadhibu kupitia maombi ya watumishi wake waaminifu.
Doreen alihisi mwisho wake umefika. Alilia kwa uchungu huku akipiga hatua za kichovu kuelekea nyumbani kwa kina Eddy kama Alivyoambiwa na Dorice ili akajisalimishe na kuombs msamaha.
Safari ilikuwa ndefu kwa binti yule aliyeuwa watu wengi shuleni kwao na kuwadhuru walimu wake wasiokuwa na hatia.
Hakuwahi kufika nyumbani kwa akina Eddy lakini alifika bila kupenda.
Umati wa watu uliokuwa nyumbani kwa mr Aloyce uliongezeka zaidi baada ya Doreen kufika pale.
Kulizuka hali ya tafrani katika eneo lile.
"Mimi ndo Maimuna halisi... Sio mama Eddy kama ulivyodhani.." Alisema Maimuna akiwa na sura mbaya kupita kiasi. Alikuwa ni mweusi mithili ya mkaa wa chunya, macho makubwa makali, mekundu kama pilipili, alikuwa na tumbo kubwa sana lililojaa michiriz, nywee zilikuwa chafu tena zimesokotana sana huku midomo yake mipana myeusi ikiyasitiri meno yake yaliyokaa hovyohovyo kinyani mwake.
Mr Aloyce aliishiwa nguvu, alishindwa kulia akadhindwa kuongea akabaki kimya amejiinamia.
Ujio wa Doreen na umati mwingine wa watu ukawa utata mwingine kwa Mr Aloyce.
"Nisamehe Eddy..." Alisikika Doreen akilia kwa sauti na wakati huo Eddy alikuwa anatembea taratibu kutokea ndani na kuja kymushuhudia kinachoendelea. Waandishi wa habari walikuwa wengi wakipiga picha tukio lile la ajabu.
Itaendelea....
Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 36 na 37

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 36 & 37
MTUNZI:ENEA FAIDY
...Mama Eddy alitazama juu ili kuona kama kuna chochote lakini hakuona kitu. Ilimbidi atumie nguvu zake za uchawi alizokuwa Nazo ili kujilinda kwani aliziona dalili za kuvamiwa katika mazingira ya kutatanisha.
Mama Eddy ambaye jina lake halisi alijulikana kama Maimuna hakuwa Mtu wa kawaida Bali alitumwa na uongozi mkuu wa himaya aliyotokea Doreen ili kumsaidia kupata vitu alivyovihitaji.
Alitumia mbinu ya kujifanya mke wa Mr Aloyce ili kuweza kumteka vizuri na kumfanya asihangaike sana kuhusu mwanae kwani kulikuwa na uwezekano mkubwa sana wa kuharibu kazi. Maimuna alikuwa ni kijakazi mkongwe wa Bi Tatile na alikuwa akiaminika sana katika himaya ya Wanatatile kwani ni mtu pekee aliyewahi kufanikisha ajali kubwa ya mabasi mawili iliyoua abiria wote kisha wakafanywa kitoweo katika sikukuu ya kumpongeza Bi Tatile kama kiongozi bora wa wachawi wote Afrika Mashariki. Bi Maimuna alikuwa akiaminika sana kwa kila kazi anayoagizwa kwani hakuwahi kufanya makosa zaidi ya tukio moja tu la kuanguka kanisani akiwa katika harakati za kuwanga mchana.
"Maimuna! Maimuna! Hapa sio kwako na Leo ndio mwisho wa ubaya wako kwenye familia hii" ilisikika sauti nyororo isiyo na mkwaruzo hata kidogo huku ikijirudia rudia. Maimuna alibaki na mshangao wa ajabu sana, akataharuki huku akihema kwa nguvu. Akaaangaza macho kila upande pasipo kumuona mtu yeyote.
Akazidi kuchanganyikiwa sana. Ghafla wazo likamjia akilini mwake, bila kuchelewa akaamua kulifanyia kazi. Akanyoosha mkono wake wake wa kulia kisha nguvu nyingi zikamjia kama radi mkononi mwake. Bi Maimuna akaachia tabasamu mwanana akiamini hakuna kitakachomdhuru kwa wakati ule wala wakati mwingine wowote. akatulia kimya akimsubiri adui yake, lakini hakuona chochote zaidi ya ukimya mzito uliokuwa umetawala.
"Kumbe unaniogopa eeeh!" Alisema Maimuna.
"Ha ha ha! Sikuogopi Maimuna... Nakuvutia pumzi tu maana sina papara" sauti ile iliyojaa dharau ilisikika. Bi Maimuna hakutushika hata kidogo kwani alikuwa anajiamini kupita kiasi. Ghafla sura yake ikabadilika sana na kuwa sura ya kutisha sana.
Meno yakawa marefu kama mnyama mkali, kucha zikawa ndefu na Kali kama za chui anayemvamia swala, macho yake yakawa meusi huku mboni yake ikiwa nyekundu kama moto. Lengo lake lilikuwa ni kuonesha nguvu zake mbele ya adui yake ambaye hakujua ni nani. Ghafla kicheko kikali cha kutisha kilichojaa dhauri na jeuri kikasikika na kumfanya Maimuna ajione mdogo kama simimizi ilihali hamjui nana aliyemcheka.
Wakati huo huo Mlango ulifunguliwa na Mr Aloyce aliingia sebuleni pale.
"Mamaaaa" Mr Aloyce alipiga ukunga wa nguvu baada ya kumkuta mkewe akiwa na umbile la kutisha sana. Uvumilivu ulimshinda alijikuta anakimbia nje kama chizi huku akihema kwa nguvu. Mlinzi alimshangaa Mr Aloyce bila kuelewa kinachoendelea.
"Vipi bosi?" Aliuliza mlinzi huku akicheka sana. Mr Aloyce alianguka chini kama mzigo huku akihema kama Mtu aliyepanda mlima mrefu kwa kasi. Mlinzi alimsogelea na kumuuliza kilichojiri.
"Kuna maajabu humo ndani"
"Maajabu gani?"
"Mke.. Mke wangu...Ame..."
"Amefanyaje tena?" Aliuliza mlinzi kwa woga kwani alishapewa onto Kali na mwanamke yule kuwa asimfatilie kwa lolote. Lakini kabla hajasema chochote kuna kitu kiliwashtua Mr Aloyce na mlinzi wakabaki wameduwaa kwa mshangao.
******
Mama Pamela hakuwa na la kufanya zaidi ya kulia tu. Muda wote ule hakujua Doreen anaendeleaje ila kilichomshangaza ni kwanini Doreen hakwenda sebuleni kujumuika nao? Alinyanyuka kitini na kwenda chumbani kwake. Lakini ghafla mshangao wa ghafla ulimvaa mwanamama yule baada ya kukuta hali ya chumba ni mbaya sana kila kitu kilikuwa shaghalabaghala tu, ndipo machale yakamcheza, akasogelea droo anayohifadhia pesa.
"Mungu wangu!" Alishtuka mama Pamela baada yakukuta droo IPO wazi lakini haina pesa yoyote zaidi ya stakabadhi ambazo hakuwa na shida nazo wakati ule. Macho yalimtoka kwa mshangao huku akitoatoa vitu ndani ya droo ile bila kuona chochote. Akasimama wima akiwa ameshika mkono kiunoni kwa hasira
"Doreen!" Aliita kwa jazba bila kujua Doreen alikwishaondoka muda mrefu uliopita. Mama Pamela akakugua tena ili kujiridisha kama kweli pesa hazikuwamo lakini bado hakukuta pesa ndani ya droo ile wala eneo lingine chumbani mle.
Mama Pamela alichanganyikiwa sana akatoka ndani ya chumba kile na kupiga hatua za harakaharaka koridoni kuelekea chumbani kwa Doreen.
Alifika mlangoni na kufungua mlango kwa jazba kubwa. Lakini cha ajabu chumba kilikuwa kitupu na hakukuwa na mtu yeyote wala dalili za uwepo wa mtu. Mama Pamela akahamaki, akamwita Doreen kwa sauti kali lakini hakuitikia.
"Mungu wangu ina maana Doreen ametoroka na pesa au?" Alijiuliza Mama Pamela akiwa ameishiwa nguvu kabisa. Hakutaka kuamini kama binti anayemuamini kiasi kile angetenda tukio lililotokea.
Mama Pamela alitoka nje ya nyumba yake ili kumtazama vizuri Doreen. Alimtafuta pale uani na kila upande wa nyumba lakini Doreen hakuwepo. Moyo wa mama Pamela ukatawaliwa na lawama nyingi sana. Akajilaumu ni kwanini hakumsikiliza mumewe mpaka yote hayo yametokea.
Akakaa chini kibarazani huku machozi yakimchuruzika. Kila akikumbuka maneno ya mwanae roho ilimuuma zaidi, hakuwa na hamu hata ya kula. Alikuwa na simanzi nzito iliyopelekea mafuriko ya machozi usoni mwake. Alilia mpaka machozi yakamkauka akiwa pale pale kibarazani kwake. Hakutaka hata kumwona binti yake kwani uchungu ungemzidia. Kwa jinsi alivyokuwa akimpenda na kumjali Pamela hakuamini kirahisi kuwa Leo amekuwa adui yake mkubwa na kumpa lawama za uchawi.
"Mungu tu Anajua" aliwaza Mama Pamela.
Majira ya saa kumi na moja jioni, Baba Pamela aliwasili jijini Mbeya na kufika nyumbani kwake akiwa na mawazo tele juu ya familia yake. Alipofika ndani tu alikutana na mkewe ambaye uso wake ulivimba sana kwa machozi ya siku nzima. Baba Pamela hakushangaa sana kwani alihisi mkewe anamlilia binti yao Pamela kumbe si hivyo tu, Bali alikuwa na jambo zito lililomtatiza sana moyoni mwake.
****
Familia ya akina Dorice ikiwa bado imekaa kikao babu yake Dorice aliyefahamika kama Mganga Tawi La Mtawile alikuwa tayari ametoa wazo kuwa atafanya jambo.
Familia nzima ikaondoka kwenye nyumba ya mama Dorice na kwenda moja kwa moja kwa Mganga Tawi la Mtawile ili kujua Dorice yupo wapi na katika hali gani.
Na kwakuwa hapakuwa mbali sana, walitumia mwendo wa dakika tano tu mpaka kufika kwenye nyumba ta Tawi La Mtawile.
Mganga yule maarufu mkoani singida, alikuwa ametenga eneo maalum nyumbani kwake kwaajili ya shughuli za uganga. Alipanga vyema vibuyu na dawa zake pembeni alizungushia kaniki nyeusi na nyekundu. Akavua viatu, kisha akawaamrisha wote waliombatana nae wavue viatu ndipo wakae kwenye zulia alilotandika chini. Wote wakafata kama walivyoamriwa.
Mganga Tawi alianza kuimba nyimbo za kuita mizimu na kuongea maneno ambayo wengine hawakuyaelewa . alitumia dakika kumi nzima kisha akachukua kioo kikubwa, akanyunyiza dawa na kuipakaza vizuri kwa kutumia mkia kama wa ng'ombe. Akaita jina la Dorice Mara tatu. Baada ya muda mfupi ardhi ikatetemeka sana radi zikapiga mfulululizo na kuwafanya wote waogope. Na kila mmoja alitamani kukimbia kwani palikuwa na utisho wa ajabu....
Riwaya:Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) -:Sehemu ya 37
....ukimya mzito ulitawala huku ndugu zake Dorice wakijiuliza ni mini kitatokea. Ghafla moshi mweusi ulioambatana na radi ukatokea mbele yao karibu na mti mdogo uliokuwa karibu na kile kijumba cha uganga cha Tawi La Mtawile. Wote wakakaza macho kwa woga huku wakitazama kwa makini moshi ule ulitokana na nini ilhali hakuna moto wowote katika eneo lile.
Kwa namna ya ajabu na ya kustaabisha sana ambayo hakuna aliyeitarajia. Doreen alitokea mbele yao akiwa na muonekano tofauti na waliomzoea. Alikuwa ni mrembo kupita kiasi huku marashi makali yenye harufu nzuri yakizidi kuziumiza pua zao kwa fujo, mikufu ya dhahabu ilining'nia shingoni mwake ikienda sambamba na hereni ilizokuwa amezivaa pamoja na Pete kwenye vidole vyake. Kila mmoja alionesha mshangao wa ajabu kwani hawakuelewa ni kwanini Dorice yupo vile. Walitulia kimya huku woga ukiwazidia kwani walijua ni mzimu wa Dorice.
"Dorice umekuwa jini?" Aliuliza Tawi la Mtawile kwa sauti Kali. Dorice akajiweka sawa na kuachia tabasamu mwanana huku akipiga hatua chache kuwasogelea ndugu zake ingawa hakuwa nao karibu sana.
"Kwanza kabisa nimefurahi kuwaona ndugu zangu... Mama nilionana nae tangu akiwa kwenye basi.." Alisema Dorice kwa sauti tulivu sana. Maneno yake yalimshtua sana Mama Dorice na kumfanya akumbuke matukio yote yaliyomtokea alipokuwa kwenye basi na kabla ya kuingia kwenye basi.
"Ni wewe?? Kwanini umekuwa jini?" Alisema Mama Dorice kwa sauti iliyojaa woga sana.
"Mimi sio jini ila ninataka kulipa kisasi na kuwakomboa watu wasio na hatia.." Alisema Dorice.
Baada ya Dorice kusema vile Wote wakatazamana kwa mshangao sana, mama Dorice alitaman mwanae Arudi katika hali ya kawaida ili aendelee kuishi nae lakini Dorice asingekubali hata kidogo kupoteza malengo yake aliyopangilia kuyafanya kwa wakati ule.
"Mama ninakupenda sana! Nina imani nitarudi nyimbani baada ya kumaliza kazi yangu... Asanteni kwa kuniita... Kwaherini!" Aliema Dorice kwa huzuni kubwa huku neno kwaheri likijirudia Mara kadhaa mpaka Alipopotea na kutoonekana tena machoni mwao. Huzuni ikamtanda mama Dorice akamtazama Mganga Tawi la Mtawile na kwa bahati wakagongana macho kwa mganga pia alikuwa akimtazama mama Dorice.
"Baba Naomba mwanangu arudi.." Alisema Mama Dorice huku chozi likimlengalenga machoni.
"Mmh! Hilo haliwezekani mwanangu... Dorice hakuwa duniani Bali aliolewa na jini na amepewa nguvu za kijini ambazo ni tishio sana... Ni kubwa kuliko kawaida na nadhani kuna jambo muhimu amekuja kulifanya maana lasivyo asingerudishwa duniani... Tawii..Tawi La Mtawileeee..!"
Alisema mganga yule kwa sauti Kali ya kiganga.
"Inamaana atakuwa jini?"
"Inawezekana akawa MTU wa ujinini siku zote"
"Eeh Mungu wangu" alisema Mama Dorice.
Mganga hakuwa na la kufanya juu ya Dorice. Wanaukoo wote walistaajabu lakini hawakuwa na la kufanya zaidi ya kupigwa na butwaa. Mama Dorice alikuwa haamini kilichomtokea mwanawe lakini hakuwa na jinsi na maneno ya mganga yalizidi kumpa mawazo mengi.
Haukupita muda sana wote walitawanyika na kwenda majumbani mwao huku suala la Dorice likiwa gumzo akilini mwao.
****
"Mama Pamela unakumbuka nilikuambia nini kuhusu mgeni wako?" Aliuliza Baba Pamela.
"Nakumbuka mume wangu" alijibu mama Pamela huku akilia. Na alijua fika kwa jinsi Baba Pamela alivyompenda mwanae basi lazima atafanya kitu kulingana na tuhuma zile alizoshtakiwa na mwanae.
"Umeona maisha mlioishi tangu amekuja?"
"Ndio.. "
"Vizuri...hebu muite hapa.."
"Hayupo... Nimemtafuta sijamwona..." Alisema Mama Pamela huku aibu na hofu vikizidi kumvamia kwa kasi sana kwani usemi usemao Asiye Sikia La Mkuu huvunjika guu ulitimia kwake kwa wakati ule ingawa hakuwa na imani kama Aliyemtoa titi binti yake alikuwa Doreen.
"Hayupo? Ameenda wapi?"
"Sijui...sijuii ameto...ametoroka... Na pesa amechukua!"
"Umeona sasa mke wangu? Umeona faida za ubishi e??"
"Nisamehe mume wangu..."
"Nilishakusamehe ila nilikuacha ujifunze.. Ila roho inaniuma sana kwa binti yangu.." Alisema Baba Pamela kwa huzuni. Maneno yake yaliibua tumaini jipya kwa mama Pamela na yakawa faraja tosha kwake. Lakini Pamela akawa kikwazo sana kwake kwani bado alikazania msimamo wake kuwa mama yake ndiye aliyemroga na kuchukua titi lake.
"Pamela mwanangu... Mama yako hawezi kufanya hivyo isipokuwa mwanazaya yule asiye na haya... Nilimwona tangu alipifika hapa ya kwamba ni mchawi ila mke wangu hakuelewa... Alimwamini sana binti yule mwenye sura ya kondoo kumbe chui"alisema Baba Pamela kwa sauti iliyojaa busara ya hali ya juu.
"Unamtetea mama.."
"Simtetei ila utaujua ukweli tu... Naamini Mungu wa Mbinguni atafanya muujiza wake hapa na lazima aliyekutenda hivi adhalilishwe.. In Jesus Name" alisema Baba Pamela mwanaume aliyekuwa anamcha Mungu kupita kiasi, alikuwa ni mwaminifu sana katika masuala ya Mungu kupita kiasi.
*****
Mr Aloyce na Mlinzi walistaajabu sana baada ta kumuona Mama Eddy (maimuna) akitoka nje mbio akiwa hajavaa nguo yoyote huku akihema kwa nguvu na kupiga mayowe hovyo.
"Nimekosaaa! Nimekosaaa" alilalama Mama Eddy huku akianguka chini na kujigaragaza kama mtu anayecharazwa viboko na nyaya za umeme.
Mr Aloyce na mlinzi walibaki wakiwa wamepigwa butwaa. Kila mmoja alishindwa la kufanya zaidi ya kumtazama tu mwanamke yule aliyeendelea kupiga kelele sana.
"Sirudiiii!sirudiiii nasema..." Alizidi kupiga kelele.
"Bosi kwani mama ana nini?" Aliuliza mlinzi.
"Unaniuliza nini na wewe si unamuona?" Alijibu Mr Aloyce.
Mama Eddy alihangaika kwa muda mrefu pale nje. Mr Aloyce aliingia ndani na kuchukua upande wa khanga ili akamsitiri mkewe lakini kila alipotaka kumfunika mkewe alikimbia kama chizi pale nje hakutaka hata kujifunika kwani alikuwa akiadhibiwa kupita kiasi bila kumuona MTU aliyemwadhibu. Mr Aloyce ilibidi atulie tuli na kumuacha mkewe aendelee kutaabika kwani yeye hakuwa na la kufanya.
Baada ya muda mrefu kupita. Mama Eddy akaanza kutulia kidogo huku akihema kwa nguvu lakini aliongea maneno ambayo hakuna aliyemwelewa.
"Mke wangu kulikoni?" Alisema Mr Aloyce kwa huruma.
"Nisamehe"
"Nikusamehe nini?"
"Nisamehe Mr Aloyce"
Mama Eddy aliendelea kuomba msamaga bila kutaja kosa lake alilolifanya. Na akiwa amekaa pale chini ghafla akaendelea kuisikia sauti iliyokuwa inamwongelesha tangu alipokuwa ndani.
"Na hapo bado... Mpaka mlipie mateso mliyowatesa watu wasio na hatia" "sirudii tafadhali" alisema mama Eddy huku akipiga magoti.
Mlinzi Na Mr Aloyce walishindwa kumuelewa Mama Eddy kwani walihisi anazungumza peke yake .
"Hurudii nini?" Aliuliza Mr Aloyce.
"Naomba nikwambie ukweli baba Eddy...mimi....!" Alisema Mama Eddy.
Wakati huo mlinzi yule alikuwa akiwaza vitisho alivyotishwa na mwanamke yule pindi alipofika nyumbani pale.
'Mh kumbeee ni mchawii' aliwaza mlinzi.
"Ukweli upi" aliuliza Mr Aloyce kwa mshangao kwani katu hakujua kama kuna kitu kinaendelea nyuma ya pazia...
Itaendelea...
Read More...