RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA NNE

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Nne
Mtunzi: Enea Faidy
Ilipoishia sehemu ya tatu ( kama hukuisoma BOFYA HAPA  )
Dorice akamsogelea Doreen kwa hatua chache.
"Jana ulikuwa na nani pale kwenye mti usiku?" aliuliza Doreen huku akiuchezesha mguu wake wa kulia chini na mkono mmoja akiwa kaushika kiunoni.
"hukuniona au?" aliuliza Dorice kwa mshangao.
"jibu swali!"
"OK! nilikuwa na Eddy"
"nani yako Eddy?"
"Doreen unanitisha ujue?"
"kha! nakutisha nina mapembe hapa? nijibu swali langu"
"Eddy mpenzi wangu!"
"nimekupata sasa... tangu lini Eddy mpenzi wako hujui kama ni mume wangu mtarajiwa?"
"Ati nini....... Eddy ni. .."
 Sehemu ya nne
.... DORICE alishtuka sana kusikia Eddy ni mume mtarajiwa wa Doreen hakutaka kuyaamini maneno ya Doreen hata kidogo.
"hivi we Doreen umechanganyikiwa au upo timamu?" Dorice aliropoka kwa hasira.
" nikuulize wewe, hivi upo timamu au mwendawazimu unavomng'ang'ania mpenzi wangu Eddy? mpaka watu wanakushangaa! inaniuma sana Dorice usione nimekukaushia!" Alisema Doreen kwa msisitizo wa hali ya juu. Maneno ambayo yalizidi kumuumiza Dorice mpaka machozi yakaanza kumlengalenga machoni mwake. Alimtazama Doreen kwa hasira huku akiumanisha meno yake kwa ghadhabu, moyoni alitamani kumuadhibu vikali Doreen kwa kutaka kulitia DOA penzi lake na Eddy lakini hakuwa na uwezo huo.
"Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako! sitaki kuamini kama rafiki yangu kipenzi Leo unageuka adui yangu!"alisema Dorice huku akipiga hatua na kutaka kuondoka mbele ya mbaya wake. Lakini ghafla Doreen akamvuta shati na kumrudisha pale alipokuwa amesimama.
"we vipi? hebu niache niondoke?"
"nitakuachaje sasa wakati unaniharibia penzi langu na Eddy?" alisema Doreen kwa kujiamini sana huku akibetua midomo yake kwa dharau utadhani Eddy ni mpenzi wake kweli kumbe hakuna lolote ni tamaa na wivu vinavyomsumbua.
"umefanikiwa kuniumiza moyo wangu Doreen mpaka najuta kukufahamu.... haya Fanya lolote utakalo tena ili kunyang'anya haki yangu ya mapenzi... do it!" alisema Dorice kwa kwikwi kwani alishindwa kuzuia kilio chake kutokana na maumivu makali aliyoyapata moyoni mwake kwani maneno ya Doreen yalikuwa kama mkuki wenye sumu katikati ya moyo wake.
"hata Mimi najuta kukutana na mwanaharamu wewe, Kwa usalama wako achana na Eddy... sijui unanielewa?"
Dorice hakusema chochote zaidi ya kumkazia macho ya hasira Doreen, bila kujua kuwa kutazamana na Doreen kwa wakati ule ilikuwa ni kujikaanga kwa mafuta yake mwenyewe kwani Doreen aliitumia nafasi ile vizuri sana.
Alijibadilisha macho yakawa ya kutisha sana kisha kila alipomtazama Dorice machoni alimhamishia vitu Fulani visivyoeleweka, kisha baada ya hapo Doreen alimsogelea Dorice na kumzodoa lakini haikuwa kumzodoa kwa kawaida Bali alimpaka vitu kama kamasi USO mzima na kumfanya Dorice atie kinyaa sana bila yeye mwenyewe kujitambua.
"hebu niondokee hapa mpuuzi wewe na ushukuru Mungu sijakufanya kitu kibaya" alisema Doreen baada ya kuhakikisha amekamilisha kazi yake aliyokusudia kwani sio siri Doreen alipania kumpata Eddy kwa vyovyote vile.
Dorice alitembea taratibu na kumfuata Eddy darasani huku akiendelea kulia.
**********
Walimu wote walikuwa hawaelewi mambo yanayoendelea shuleni pale, kwani kila siku liliibuka jipya. Suala la mwalimu John kuvuliwa suruali kwa mazingira ya kutatanisha lilizidi kuwapa maswali mengi walimu wa while ya sekondari mabango mpaka wakaogopa hata kuingia madarasani, kwani walihisi wanaweza kudhalilishwa kama ilivyomtokea mwalimu John.
Mbali na suala hilo pia suala la mkuu wa shule kujifungia ofisini liliwapa mtihani mkubwa kwani haikuwa kawaida yake.
"jamani nimeenda ofisi ya mkuu wa shule karibia Mara tatu nimegonga sana lakini hakutoa jibu hata nilipojaribu kusukuma mlango inaonekana amefunga kwa ndani!" alisema makamu mkuu wa shule baada ya kuingia staff.
"hata Mimi nimeenda pale ofisini lakini palikuwa kimya sana ingawa mlango unaonekana umefunguliwa kwa nje... nimepiga simu haipokelewi" alisema mtaaluma.
kiukweli iliibuka sintofahamu miongoni mwa walimu wote waliingiwa na hofu kubwa.
" mmh! hii sio kawaida ya mkuu kabisa inabidi tufanye jambo"
"Mimi naona tuvunje mlango tu" alipendekeza mwalimu wa nidhamu.
walimu wote walikubaliana kuvunja mlango wa ofisi ya mkuu wa shule. wakaebda moja kwa moja mpaka ofisini kwa mkuu na kuvunja mlango kisha wakaingia.. walichokutana nacho kila MTU hakuamini , walibaki midomo wazi huku machozi yakiwadondoka kama chemichemi katikati ya mlima.
Mwili wa mwalimu Mbeshi ulikuwa umeoza vibaya sana funza walitapakaa kila mahali wakisindikizwa na harufu mbaya iliyojaa ofisini mle. hakuwa mbeshi tena mwanamama aliyejipenda na kunukia marashi muda wote Bali jina lilibadilika na kuwa maiti.
Walimu walitulia kimya kwa muda wa dakika mbili nzima Vila kusema chochote lakini macho ya makamu mkuu wa shule yalitua mpaka mezani kwa mbeshi ambapo aliona karatasi ndogo nyeupe yenye ujumbe. Akaisogelea na kuichukua, kisha akaanza kuisoma. Ghafla alishtuka sana baada ya kusoma ujumbe ule "UNAFATA WEWE ULIYESOMA KARATASI HII."
Makamu yule kwa woga na hamaki akaropoka " Mimi sijasoma chochote... tusisingiziane hapa!" alisema huku akificha macho yake na kumkabidhi mtaaluma karatasi ile kwani walimu wote hawakujua kilichotokea hivyo wakatamani wasome ujumbe uliokuwemo mle.
********
Dorice alimtuma MTU amwitie Eddy darasani lakini mwanafunzi yule akakataa. hivyo Doreen aliamua kwenda mwenyewe darasani mle.
Darasa lilikuwa limetulia kimya sana, Dorice akafungua mlango na kuingia lakini ghafla alipoingia wanafunzi wote darasani mle wakacheka kicheko kikali sana kilichomtia hofu sana Dorice. lakini akajikaza kisabuni licha ya kwamba alijua wanamcheka yeye, akamsogelea Eddy na kumtaka watoke nje lakini Dorice aligundua mabadiliko makubwa sana kwa Eddy Ila hakuuliza chochote wakatoka nje. wanafunzi wakacheka tena kwa dharau kitendo kilichomuumiza sana Dorice.
"hivi we demu unajisoma??" alisema Eddy kwa ukali. maneno hayo yalimshtua sana Dorice.
"Eddy! sijakuelewa!"
" unajisoma kweli? hivi kwanza unajua majamaa wanakucheka kwa sababu gani?" maneno ya Eddy yalimfanya Dorice ataharuki.....
Itaendelea ......RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Nne
Mtunzi: Enea Faidy
Ilipoishia sehemu ya tatu ( kama hukuisoma bofya hapa )
Dorice akamsogelea Doreen kwa hatua chache.
"Jana ulikuwa na nani pale kwenye mti usiku?" aliuliza Doreen huku akiuchezesha mguu wake wa kulia chini na mkono mmoja akiwa kaushika kiunoni.
"hukuniona au?" aliuliza Dorice kwa mshangao.
"jibu swali!"
"OK! nilikuwa na Eddy"
"nani yako Eddy?"
"Doreen unanitisha ujue?"
"kha! nakutisha nina mapembe hapa? nijibu swali langu"
"Eddy mpenzi wangu!"
"nimekupata sasa... tangu lini Eddy mpenzi wako hujui kama ni mume wangu mtarajiwa?"
"Ati nini....... Eddy ni. .."
 Sehemu ya nne
.... DORICE alishtuka sana kusikia Eddy ni mume mtarajiwa wa Doreen hakutaka kuyaamini maneno ya Doreen hata kidogo.
"hivi we Doreen umechanganyikiwa au upo timamu?" Dorice aliropoka kwa hasira.
" nikuulize wewe, hivi upo timamu au mwendawazimu unavomng'ang'ania mpenzi wangu Eddy? mpaka watu wanakushangaa! inaniuma sana Dorice usione nimekukaushia!" Alisema Doreen kwa msisitizo wa hali ya juu. Maneno ambayo yalizidi kumuumiza Dorice mpaka machozi yakaanza kumlengalenga machoni mwake. Alimtazama Doreen kwa hasira huku akiumanisha meno yake kwa ghadhabu, moyoni alitamani kumuadhibu vikali Doreen kwa kutaka kulitia DOA penzi lake na Eddy lakini hakuwa na uwezo huo.
"Ama kweli kikulacho ki nguoni mwako! sitaki kuamini kama rafiki yangu kipenzi Leo unageuka adui yangu!"alisema Dorice huku akipiga hatua na kutaka kuondoka mbele ya mbaya wake. Lakini ghafla Doreen akamvuta shati na kumrudisha pale alipokuwa amesimama.
"we vipi? hebu niache niondoke?"
"nitakuachaje sasa wakati unaniharibia penzi langu na Eddy?" alisema Doreen kwa kujiamini sana huku akibetua midomo yake kwa dharau utadhani Eddy ni mpenzi wake kweli kumbe hakuna lolote ni tamaa na wivu vinavyomsumbua.
"umefanikiwa kuniumiza moyo wangu Doreen mpaka najuta kukufahamu.... haya Fanya lolote utakalo tena ili kunyang'anya haki yangu ya mapenzi... do it!" alisema Dorice kwa kwikwi kwani alishindwa kuzuia kilio chake kutokana na maumivu makali aliyoyapata moyoni mwake kwani maneno ya Doreen yalikuwa kama mkuki wenye sumu katikati ya moyo wake.
"hata Mimi najuta kukutana na mwanaharamu wewe, Kwa usalama wako achana na Eddy... sijui unanielewa?"
Dorice hakusema chochote zaidi ya kumkazia macho ya hasira Doreen, bila kujua kuwa kutazamana na Doreen kwa wakati ule ilikuwa ni kujikaanga kwa mafuta yake mwenyewe kwani Doreen aliitumia nafasi ile vizuri sana.
Alijibadilisha macho yakawa ya kutisha sana kisha kila alipomtazama Dorice machoni alimhamishia vitu Fulani visivyoeleweka, kisha baada ya hapo Doreen alimsogelea Dorice na kumzodoa lakini haikuwa kumzodoa kwa kawaida Bali alimpaka vitu kama kamasi USO mzima na kumfanya Dorice atie kinyaa sana bila yeye mwenyewe kujitambua.
"hebu niondokee hapa mpuuzi wewe na ushukuru Mungu sijakufanya kitu kibaya" alisema Doreen baada ya kuhakikisha amekamilisha kazi yake aliyokusudia kwani sio siri Doreen alipania kumpata Eddy kwa vyovyote vile.
Dorice alitembea taratibu na kumfuata Eddy darasani huku akiendelea kulia.
**********
Walimu wote walikuwa hawaelewi mambo yanayoendelea shuleni pale, kwani kila siku liliibuka jipya. Suala la mwalimu John kuvuliwa suruali kwa mazingira ya kutatanisha lilizidi kuwapa maswali mengi walimu wa while ya sekondari mabango mpaka wakaogopa hata kuingia madarasani, kwani walihisi wanaweza kudhalilishwa kama ilivyomtokea mwalimu John.
Mbali na suala hilo pia suala la mkuu wa shule kujifungia ofisini liliwapa mtihani mkubwa kwani haikuwa kawaida yake.
"jamani nimeenda ofisi ya mkuu wa shule karibia Mara tatu nimegonga sana lakini hakutoa jibu hata nilipojaribu kusukuma mlango inaonekana amefunga kwa ndani!" alisema makamu mkuu wa shule baada ya kuingia staff.
"hata Mimi nimeenda pale ofisini lakini palikuwa kimya sana ingawa mlango unaonekana umefunguliwa kwa nje... nimepiga simu haipokelewi" alisema mtaaluma.
kiukweli iliibuka sintofahamu miongoni mwa walimu wote waliingiwa na hofu kubwa.
" mmh! hii sio kawaida ya mkuu kabisa inabidi tufanye jambo"
"Mimi naona tuvunje mlango tu" alipendekeza mwalimu wa nidhamu.
walimu wote walikubaliana kuvunja mlango wa ofisi ya mkuu wa shule. wakaebda moja kwa moja mpaka ofisini kwa mkuu na kuvunja mlango kisha wakaingia.. walichokutana nacho kila MTU hakuamini , walibaki midomo wazi huku machozi yakiwadondoka kama chemichemi katikati ya mlima.
Mwili wa mwalimu Mbeshi ulikuwa umeoza vibaya sana funza walitapakaa kila mahali wakisindikizwa na harufu mbaya iliyojaa ofisini mle. hakuwa mbeshi tena mwanamama aliyejipenda na kunukia marashi muda wote Bali jina lilibadilika na kuwa maiti.
Walimu walitulia kimya kwa muda wa dakika mbili nzima Vila kusema chochote lakini macho ya makamu mkuu wa shule yalitua mpaka mezani kwa mbeshi ambapo aliona karatasi ndogo nyeupe yenye ujumbe. Akaisogelea na kuichukua, kisha akaanza kuisoma. Ghafla alishtuka sana baada ya kusoma ujumbe ule "UNAFATA WEWE ULIYESOMA KARATASI HII."
Makamu yule kwa woga na hamaki akaropoka " Mimi sijasoma chochote... tusisingiziane hapa!" alisema huku akificha macho yake na kumkabidhi mtaaluma karatasi ile kwani walimu wote hawakujua kilichotokea hivyo wakatamani wasome ujumbe uliokuwemo mle.
********
Dorice alimtuma MTU amwitie Eddy darasani lakini mwanafunzi yule akakataa. hivyo Doreen aliamua kwenda mwenyewe darasani mle.
Darasa lilikuwa limetulia kimya sana, Dorice akafungua mlango na kuingia lakini ghafla alipoingia wanafunzi wote darasani mle wakacheka kicheko kikali sana kilichomtia hofu sana Dorice. lakini akajikaza kisabuni licha ya kwamba alijua wanamcheka yeye, akamsogelea Eddy na kumtaka watoke nje lakini Dorice aligundua mabadiliko makubwa sana kwa Eddy Ila hakuuliza chochote wakatoka nje. wanafunzi wakacheka tena kwa dharau kitendo kilichomuumiza sana Dorice.
"hivi we demu unajisoma??" alisema Eddy kwa ukali. maneno hayo yalimshtua sana Dorice.
"Eddy! sijakuelewa!"
" unajisoma kweli? hivi kwanza unajua majamaa wanakucheka kwa sababu gani?" maneno ya Eddy yalimfanya Dorice ataharuki.....
Itaendelea ......

Related Post

Previous
Next Post »