About KABENDE.COM

Manual Description Here: Ea eam labores imperdiet, apeirian democritum ei nam, doming neglegentur ad vis.

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 27

RIWAYA:A WIZARD STUDENT (MWANAFUNZI MCHAWI)

MTUNZI: ENEA FAIDY

SEHEMU YA 27

...... MR ALOYCE alibaki kimya akiwa ametulia kimya kama vile amegandishwa na gundi ngumu. Haja ndogo ilipita taratibu katikati ya mapaja yake na kushuka chini ardhini. Alitamani ardhi ipasuke ili walau akajifiche chini ya ardhi kuliko kuendelea kushuhudia tukio lililokuwa linaendelea kwa wakati ule. Akili ilisimama, mwili ulinyong'onyea kwani hakuwa na lolote la kuweza kufikikiria kwa wakati ule. "Nimekamatika kwenye mtego" ndilo wazo pekee lililomjia akilini mwake.
Chatu yule aliendelea kujiviringisha kwa madaha na mbwembwe nyingi mwilini mwa Mr Aloyce na kumfanya mwanaume yule ajihisi mfu aliyebakisha roho yake tu kabla ya mazishi. "Nisaidie Mungu wangu" Mr Aloyce alisali kimoyo moyo akiamini kwamba huenda Mungu atasikia maombi yake na kumkumkumbuka katika Mateso yake. Machozi hayakumtoka hata chembe kwani hofu ilimzidia mpaka chozi lilimkauka.
Akiwa katika hali hiyo ngumu isiyoelezeka Mr Alloyce hakuona mtu yeyote wala dalili ya kiumbe chochote katika eneo lile. Ghafla upepo mkali ukapuliza eneo lile, ulikuwa kama kimbunga kinachoweza kuleta maafa kwa makazi ya watu. Mr Aloyce alijishangaa sana kuona mwili wake ukiwa mwepesi sana tena umejiachia kupita kiasi. Moyo wake ukafurahi na akatumia nafasi hiyo kujitazama mwilini mwake, akagundua yule chatu hayupo tena mwilini mwake Bali amesogea pembeni kidogo na kujituliza kama gogo.

Macho yalimtoka kama njugu akimtazama yule Chatu, ghafla akapigwa na mshangao wa ajabu baada yule chatu kubadilika umbile na kuwa na umbo la mtu. Mr Alloyce akamkazia macho MTU yule aliyetokana na chatu. Hakuamini macho yake pale alipogundua mtu yule alikuwa mkewe, Aloyce alitetemeka sana. Ndipo mwanamke yule alipoachia kicheko kikali sana huku akimsogelea Mr Aloyce. "Nilikukumbuka sana mume wangu.. Ila nasikitika unaniogopa" alisema mwanamke yule mwenye sura na umbile la mama Eddy. Mr Aloyce alitetemeka sana, akapiga hatua za kinyumenyume kumkwepa mwanamke yule.
"Mume wangu! Mbona unaniogopa?" Alisema mwanamke yule.

****

Dorice alimtazama Mansoor na kumsikiliza kwa umakini huku akiwa na hamu kubwa ya kutaka kujua njia nyingine ya kuweza kuondoka katika himaya ile ya kijini na kurudi duniani ili kumkomboa Eddy mpenzi wake wa dhati.
Mansoor alimtazama Dorice kwa unyonge sana, sura yake ilidhihirisha huzuni aliyokuwa nayo moyoni mwake. Akasogeza mkono wake na kuushika mkono wa Dorice kisha akausogeza karibu kabisa na midomo yake mizuri. Akaachia mabusu mazito mfululizo huku chozi likimdondoka. Kisha akainua macho yake na kumtazama Dorice.
"Dorice kwanini hunipendi?" Aliuliza Mansoor. Dorice alimtazama Mansoor bila kujibu chochote.
"Kwanini hunipendi?" Aliuliza tena Mansoor huku macho yake yakizidi kuwa mekundu kama pilipili. Kisha taratibu machozi yake yalianza kubadilika rangi na kuwa kama damu.
"Dorice! Naumia sana moyoni mwangu kumpenda mtu asiyenipenda! Najilaumu sana ingawa sio kosa language ila ni kosa la moyo wangu ambao haukumchagua yeyote ila wewe.. Natamani ungejua thamani ya upendo wangu kabla haujaenda duniani ili unikumbuke moyoni mwako" alisema Mansoor huku machozi mekundu yakizidi kudondokea kwenye mikono mizuri na laini ya Dorice. Maneno Yale yaliugusa moyo wa Dorice, akahisi ni mkosaji sana kwa kuutesa moyo wa Mansoor. Machozi yalimlengalenga machoni mwake akajikuta anamkumbatia Mansoor na kumtakia maneno ambayo hakuwahi kumtamkia hata Mara moja.
"NAKUPENDA SANA MANSOOR" alisema Dorice huku midomo yake ikibusu shingo ya Mansoor kwa huba, na mikono yake ilitembea taratibu mgongoni kwa Mansoor na macho yake yalikuwa yamefumba na kumpa nafasi zaidi ya kuzitafakari kwa kina hisia za mapenzi zilizokuwa kichwani mwake.
"Asante sana mpenzi wangu... Nakupenda na nitazidi kukupenda milele.." Ilisikika sauti iliyojaa huba na mahaba mazito ya Mansoor.
"Asante mpenzi... Lakini naomba unisaidie kwa lile suala langu.. Na umesema kwamba kuna njia nyingine.." Alisema Dorice akiwa bado amemkumbatia Mansoor.
Swali lile lilikuwa kero kwa Mabsoor kwani alijua Dorice hatozungumzia tens suala lile baada ya kumpa maneno matamu zaidi ya asali.
"Mh! Nitakusaidia... " alisema Mansoor.
"Lini?"
"Kuwa na subira... Wala usijali... " Mansoor alimwondoa shaka Dorice. Baada ya muda mfupi Mansoor alimuaga Dorice kisha akatoweka machoni pake huku akimuahidi kuwa atarudi baada ya muda mfupi tu. 
Hazikupita dakika nyingi Mansoor alijitokeza tena kwa Doreen lakini alikuwa na kitu kilichomshtua Doreen na kumfanya aogope sana.

******
Siku ya kwanza ndani ya nyumba ya mama Pamela iliisha vizuri sana wakiwa na Doreen. Usiku majira ya SAA NNE baada ya kula na kutazama televisheni huku wakipiga soga za hapa na pale wakaagana na kila mmoja alienda kulala kwenye chumba chake. 
Usiku ule Mama Pamela alihisi kuna utofauti ambao hakuuzoea kabisa. 
Paka walilia Mfululizo na kumfanya Mama Pamela ahamaki kidogo, sauti ya paka kutoka batini ilisikika ikilia kama mtoto mchanga jambo ambalo lilimtisha mama Pamela. Na haikuwa hivyo kwa mama Pamela tu bali pia hata kwa Pamela kwani alikuwa anaogopa kupita kiasi.
Ghafla usingizi wa ajabu ukampitia Mama Pamela, macho yalikuwa mazito kiasi kwamba alishindwa hata kuyafumbua ingawa akili yake bado ilikuwa inaendelea kuwaza . akajishangaa na kujiuliza usingizi ule ulikuwa wa aina gani kwani kwa kawaida mtu akilala hata akili pia inalala. Ghafla kitu kizito militia juu yake, akashindwa kupumua vizuri na kila alipojaribu kujiinua alishindwa. Akahisi anakabwa sana shingoni na kila alipojaribu kuinua mkono wake ili ajiokoe alishindwa. Akazidi kuhema kwa nguvu.
Nusu SAA nzima hali ile ilizidi kumsumbua mpaka aliposhtuka na kukaa kitandani huku jasho likimtoka kwa kasi kana vile yupo jijini Dar kumbe yupo Mbeya kwenye baridi Kali. Alikaa kitandani huku akihema sana ghafla akasikia kishindo kikali sana kilichomshtua na kumfanya atahamaki. 
"Mamaaaa! Mamaa " sauti ya Pamela ilimshtua sana Bi Carolina. Akatamani ainuke kitandani pale ili akamtazame mwanaye, Mara taa ikazimwa. Akajua umeme umekatika lakini kilichomshangaza ..........

ITAENDELEA....
LIKE, COMMENT, SHAR

Read More...

NACTE Yavifutia Usajili vyuo 5 nchini , 41 vyafungiwa kuendesha mafunzo na 175 vapewa notisi ya kushushwa hadhi.

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limetangaza kuwa vyuo 5 vimefungwa kuendesha mafunzo na kufutwa kwenye rejista ya vyuo vya ufundi nchini. 

Pia Baraza limetangaza kuwa vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria vimepewa muda wa wiki mbili na kutakiwa vijisajili mara moja kwenye Baraza hilo kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
 
Vilevile, vibali vya  usajili wa vyuo 112 vya kutoa elimu ya ufundi vimefikia ukomo hivyo vinapaswa kutekeleza masharti ya Usajili; wakati  vyuo 57 vimefikia ukomo wa ithibati, hivyo inapaswa kutekeleza masharti ya ithibati, imetangazwa jana.
 
Akiongea katika mkutano na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Baraza (NACTE), Mhandisi Steven Mlote, amesema Baraza limetoa muda wa mwezi mmoja kwa vyuo 112 kutekeleza masharti ya usajili na vyuo 52 kutekeleza masharti ya ithibati kwa mujibu wa sheria za uendeshaji vyuo vya ufundi nchini, na vyuo vitakavyoshindwa kutekeleza agizo hili vitafungiwa mara moja.
 
Mhandisi Mlote pia alitoa onyo akisema “vyuo 41 vinavyotoa elimu ya ufundi bila kusajiliwa kwa mujibu wa sheria nimevipa muda wa wiki mbili na navitaka vijisajili mara moja kwenye Baraza kabla ya kuchukuliwa hatua kali za kisheria”.
 
Mhandisi Mlote alivitaja vyuo vyote vyenye matatizo kama ifuatavyo:
Jedwali I: Vyuo vya Ufundi Vilivyofutiwa Usajili
NA.
CHUO

State College of Health and Allied Sciences - Dar es Salaam

Zoom Polytechnic College - Dar es Salaam

Tabitha College – Dar es Salaam (formerly: Thabita Vocational Training College - Dar es Salaam)

Financial Training Centre - Dar es Salaam

TMBI College of Business and Finance - Dar es Salaam

Jedwali II: Vyuo ambavyo Havijasajiliwa na vinavyoendesha Programu zisizo na Kibali cha Baraza

NA.
CHUO
1.      
King Solomoni College - Arusha
2.      
Avocet College of  Hotel Management - Arusha
3.      
Kewovac Nursing Training Centre - Mbagala, Dar es Salaam
4.      
St. Family Health Training Institute - Mbagala, Dar es Salaam
5.      
Bethesda Montessori Teachers Training College - Arusha
6.      
Green Themi Teacher’s College & Green Themi Institute of Tourism
7.      
Mainland Institute of Professionals - Arusha
8.      
St. David College of Health - Dar es Salaam
9.      
Islamic Culture School - Dar es Salaam
10.   
Tanzania Education College - Dar es Salaam
11.   
Macmillan Training College - Dar es Salaam
12.   
Tanzania International University (TIU) - Dar es Salaam
13.   
Dodoma College of Business Management - Dodoma
14.   
Faraja Health and Emergencies - Mbeya
15.   
St. Joseph College - Mbeya
16.   
St. Peter Health Management - Mbeya
17.   
Kapombe Nursing School - Mbeya
18.   
Uyole Health Institute - Mbeya
19.   
Josephine Health Institute - Mbeya
20.   
Institute of Public Administration - Chake chake Pemba
21.   
Dar es Salaam College of Hotel and Business Studies - Vuga, Unguja, Zanzibar and Chake Chake, Pemba, Zanzibar
22.   
Zanzibar Training Institute, the Professional College of Information Technology, Languages and Business Studies - Mwera Meli Sita Unguja  Zanzibar
23.   
Azania College of Management - Raha Leo, Zanzibar
24.   
Time School of Journalism - Chakechake, Pemba
25.   
Residence Professional College - Mombasa, Zanzibar  
26.   
Mkolani Foundation Organisation - Mwanza
27.   
Kahama College of Health Sciences - Kahama
28.   
Institute of Adult Education-Mwanza Campus - Luchelele Site
29.   
Zoom Polytechnic - Bukoba
30.   
Johrow Star Training College - Shinyanga
31.   
St. Thomas Training College – Shinyanga
32.   
Dar es Salaam School of Journalism and Mass Communication DMSJ - Bukoba
33.   
Dar es Salaam School of Journalism and Mass Communication (DMSJ - Mwanza
34.   
Dar es Salaam School of Journalism and Mass Communication (DMSJ - Geita 
35.   
Dar es Salaam School of Journalism and Mass Communication (DMSJ - Simiyu
36.   
Harvest Institute of Health Sciences - Mwanza
37.   
Singin International - Bukoba
38.   
College of Business Management - Mombasa, Zanzibar
39.   
Tanzania Star Teachers College - Chakechake, Pemba, Zanzibar
40.   
Tanzania Star Teachers College - Unguja, Zanzibar
41.   
St. Mary's International School of Business - Sumbawanga

Jedwali III: Vyuo Vilivyosajiliwa lakini Vinatoa Programu zisizo na Kibali cha Baraza
NA.
CHUO
PROGRAMU
1.
AP and Prime College of Business Studies - Dar es Salaam
Medical Attendant
Nursing Assistant
2.
Universal College of Africa - Dar es Salaam
Banking and Finance
Business Administration
Clearing and Forwarding
Airfares
Information and Communication Technology
Nursing
Hotel Management
Secretarial Course
Procurement and Supplies
3.
Professional Skills Development International  (PSDI-CENTRE) Centre - Bagamoyo
Offering Non-NTA programmes (Various Short Courses)
4.
Ruter Institute of Financial Management - Mwanza
Accountancy
Procurement and Supply
Banking and Finance
ICT
  5.
Mwanza Polytechnic College - Maswa
Ordinary Diploma in Early Childhood Education
      6.

Royal College of Tanzania - Dar es Salaam
Law
  7.
Belvedere Business and Technology College - Mwanza
Accountancy
  8.
Chato College of Health Sciences and Technology - Chato
Pharmacy
9
St. Glory College of Health and Allied Sciences - Dar es Salaam
Medical Attendant

10.
Zoom Polytechnic College - Dar es Salaam
Computer Science

11.
Zanzibar Technology College - Zanzibar
Computer Science
Business Information System

Jendwali IV: Vyuo vyenye Hadhi ya Usajili Iliyokwisha Muda wake
NA.
CHUO

Mteule Training College - Morogoro

Favre Language and Communication Institute - Dar es Salaam

Eagle Wings Training College - Dar-es-Salaam

The Sinon College - Dar es Salaam

Green Hill Institute (GHI) - Mbeya

Institute of Business Management (IBM) - Morogoro

Modern Commercial Institute (MCI) - Dar es Salaam

Evin School of Management - Dar es Salaam

SAMFELIS College of Business Studies - Dar es Salaam

Agape College - Dar es Salaam

Belvedere Business and Technology College - Mwanza

Dar es Salaam Institute of Business Management - Dar es Salaam

Ellys Institute of Technology - Bunda

Tanzania Institute of Chartered Secretaries and Administrators (TICSA) - Arusha

Msakamali Institute of Business Studies and Technology (MIBST) - Msata

Cum Laude College - Njombe

Tarime Institute of Business Management (formerly Tarime Business Training Institute) - Tarime

Dar es Salaam College of Hotel and Business Studies - Dar es Salaam

Institute of Management and Development Studies - Iringa (Formerly: Sophist  Tanzania College - Iringa)

Greenbelt Polytechnic College - Morogoro

Zanzibar Institute of Journalism and Mass Communication (ZIJMC) - Zanzibar

Habari Media Training Centre (HAMETC) - Dar es Salaam

City Media College - Arusha

Arusha East African Training Institute - Arusha

AP and Prime College of Business Studies – Dar es Salaam

DayStar Training College - Dar es Salaam

Emmanuel Community College - Kibaha

Victoria Institute of Tourism and Hotel Management  - Mwanza

Zanzibar Professional Training Institute (ZPTI) - Zanzibar

Rungwe International College of Business and Entrepreneurship - Mbeya

Mbengwenya College of Business and Information Technology  -  Mbinga

Musoma Utalii College - Shinyanga

Dar es Salaam Institute of Journalism and Mass Communication (DIJMC) - Dar es Salaam

Ubuntu Institute of Social Justice (UISJ) - Mwanza

Institute of Skills Development (ISD) - Morogoro formerly: RK Institute of Innovations (RKII) - Morogoro)

Mbeya Training College (MTC) - Mbeya

Media and Values Training Institute (MEVATI) - Dar es Salaam

Marian College of Law (MCL) - Dar es Salaam

PCTL Training Institute (PTI) - Dar es Salaam

KAPS Community Development Institute - Mafinga, Iringa

Professional Skills Development International  (PSDI-CENTRE) Centre - Bagamoyo

East African Institute of Entrepreneurship and Financial Management (EAIEFM) - Arusha

New Focus College - Mbeya

Northern Peaks Business College (NPBC) - Arusha

Mbalizi Polytechnic College - Mbeya

Genesis School of Information Technology and Journalism - Dar es Salaam
47.   
Kiteto School of Nursing - Kibaya
48.   
Kunduchi Nursing School – Dar es Salaam
49.   
Wisdom Medical laboratory Training and Research Centre - Dodoma
50.   
Global Community College - Geita
51.   
KCMC School of Assistant Medical Officers (Radiology) - Moshi
52.   
School of Physiotherapy - Moshi
53.   
Advanced Paediatric Nursing School - Moshi
54.   
KCMC Assistant Medical Officers’ Ophthalmology School - Moshi
55.   
Advanced Ophthalmic Nursing School - Moshi
56.   
Nicodemus Hhando School of Health Sciences - Manyara
57.   
Litembo Health Laboratory Sciences School - Mbinga
58.   
Rukwa College of Health Sciences - Sumbawanga
59.   
Clinical Officers’ Training Centre - Songea
60.   
Clinical Officers’ Training Centre - Sumbawanga
61.   
Isimila Nursing School - Iringa
62.   
St. Peters Health Training Institute - Iringa
63.   
CAGETI Polytechnic College - Mafinga
64.   
Makambako Institute of Health Sciences - Makambako
65.   
Mbozi School of Nursing - Mbeya
66.   
Biharamulo Health Sciences Training College - Kagera
67.   
St. Bernard Health Training Institute - Katoro, Geita
68.   
Karagwe College of Medical Laboratory and Allied Sciences - Karagwe
69.   
Geita Medical Laboratory and Nursing Training College - Geita
70.   
Royona College of Health and Allied Sciences - Mwanza
71.   
Assistant Medical Officers’ Training Centre - Bugando
72.   
GISAN Health Training Institute - Mwanza
73.   
St. Maximilliancolbe Health College - Tabora
74.   
Sr. Dr. Thekla Nyangao School of Nursing - Lindi
75.   
Karatu Health Training Institute - Arusha
76.   
St. Peter’s College of Health Science – Dar es Salaam
77.   
St. Gaspar Nursing School - Singida
78.   
City College of Health and Allied Sciences - Dar es Salaam
79.   
Sumve School of Nursing - Kwimba
80.   
Pamoja College of  Agriculture and Livestock - Babati
81.   
Regional Aviation College - Dar es Salaam
82.   
Institute of Management and Information Technology - Dar es Salaam
83.   
Institute for Environment and Development Sustainability - Dar es Salaam
84.   
Fire and Rescue Training Centre - Dar es Salaam
85.   
TPDF IT Centre - Dar es Salaam
86.   
Zanzibar Technology College - Zanzibar
87.   
Modern Polytechnic  - Zanzibar
88.   
Community Resources Development Organisation Training Institute - Mwanza
89.   
Muleba Lutheran Vocational Training Centre - Muleba
90.   
Ministry of Agriculture Training Institute Maruku -Bukoba
91.   
Mwangaria Institute of Agriculture and Livestock - Moshi
92.   
Simanjiro Animal Husbandry Vocational Training Centre - Arusha
93.   
MATI IGURUSI - Mbeya
94.   
Kilimanjaro Agricultural Training Centre - Moshi
95.   
LITA Buhuri - Tanga
96.   
Forest Industries Training Institute (FITI) - Moshi-
97.   
Arusha Institute of Technology - Arusha
98.   
MATI Mtwara - Mtwara
99.   
National Meteorological Training Centre - Kigoma
100.                  
Visele Live-crop Skills Training Centre - Mpwapwa
101.                  
Mt. Maria Goretti College of Agriculture - Mazombe, Kilolo
102.                  
Institute of Lands – Dar es Salaam
103.                  
Horticulture Research and Training Institute (HORTI) – Tengeru, Arusha
104.                  
VETA Kipawa Information and Communication Technology – Dar es Salaam
105.                  
Gataraye Research and Training Centre – Dar es Salaam
106.                  
Nyerere Road Teacher’s College - Singida
107.                  
Bugingo Teachers College - Pwani
108.                  
Majority Teacher’s College - Mbeya
109.                  
MAM Institute of Education - Mbeya
110.                  
Victoria Unique College - Mwanza
111.                  
Mwanza Polytechnic Institute - Mwanza
112.                  
Zanzibar Education College - Zanzibar

Jedwali V: Vyuo vyenye Hadhi ya Ithibati Iliyokwisha Muda wake
NA.
CHUO
1.      
Gender Training Institute (GTI)  - Dar es Salaam
2.      
DINOBB Institute of Sciences and Business Technology -Ipinda,  Mbeya
3.      
Royal College of Tanzania (formerly: Royal College of Journalism - Dar es Salaam)
4.      
Morogoro School of Journalism (MSJ) - Morogoro
5.      
Dar-es-Salaam School of Journalism (DSJ) - Dar es Salaam
6.      
Shukrani International College of Business Management and Administration - Mbeya
7.      
Dar-es-Salaam City College (DACICO)  - Dar es Salaam
8.      
Institute of Continuing and Professional Studies – Zanzibar
9.      
Korogwe School of Nursing - Korogwe
10.   
Dental Therapists Training Centre - Tanga
11.   
Dental Therapists Training Centre - Mbeya
12.   
Assistant Medical Officers’ Training Centre - Tanga
13.   
Assistant Medical Officers’ Training Centre - Mbeya
14.   
School of Dental Therapy - Mbeya
15.   
Njombe School of Nursing - Njombe
16.   
Clinical Officers’ Training Centre - Mafinga
17.   
Kibaha Clinical Officers’ Training Centre – Coast Region
18.   
Mkomaindo School of Nursing - Masasi
19.   
Tosamaganga School of Nursing - Iringa
20.   
Newala School of Nursing - Mtwara
21.   
Mbulu School of Nursing - Manyara
22.   
Lindi Clinical Officers’ Training Centre - Lindi
23.   
Maswa Clinical Officers’ Training Centre - Shinyanga
24.   
KCMC School of Physiotherapy - Moshi
25.   
KCMC School of Advanced Paediatric Nursing - Moshi
26.   
KCMC AMO Anaesthesia School - Moshi
27.   
Geita School of Nursing - Geita
28.   
Muhimbili School of Midwifery - Dar es Salaam
29.   
Sengerema Health Training Institute - Sengerema
30.   
KAM College of Health Sciences - Dar-es-Salaam
31.   
Kilimatinde Nurses and Midwives Training School - Manyoni
32.   
Kiomboi Nurses and Midwives Training School - Iramba
33.   
Royal Training Institute - Dar-es-Salaam
34.   
Heri School of Nursing - Kigoma
35.   
College of Health Sciences Zanzibar - Zanzibar
36.   
Clinical Officers’ Training Centre - Musoma
37.   
Kagemu School of Environmental Health Sciences - Bukoba
38.   
Bugando School of Nursing - Mwanza
39.   
Ngudu School of Environmental Health Sciences - Kwimba
40.   
Lugalo Military Medical School - Dar-es-Salaam
41.   
Lugarawa School of Nursing - Ludewa
42.   
Mvumi Institute of Health Sciences - Dodoma
43.   
Masasi Clinical Assistants Training Centre - Masasi
44.   
Ndanda Nursing School - Masasi
45.   
Massana College of Nursing - Dar-es-Salaam
46.   
Machame Health Training Institute - Kilimanjaro
47.   
Vector Control Training Centre - Muheza
48.   
Operating Theatre Management School - Mbeya
49.   
Tarime School of Nursing - Tarime
50.   
Bandari College – Dar es Salaam
51.   
Civil Aviation Training Centre - Dar es Salaam
52.   
Institute of Wildlife Management Pasiansi - Mwanza


Imetolewa na:
KAIMU KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI (NACTE)
TAREHE: 3 AGOSTI 2016
Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 26

RIWAYA:A WIZARD STUDENT (MWANAFUNZI MCHAWI)
MTUNZI: ENEA FAIDY
SEHEMU YA 26
..BI CAROLINA alipiga hatua za taratibu kuelekea sebuleni lakini hali iliyokuwemo ndani mle ilizidi kumshangaza kwani alisikia harufu
Read More...

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha dodoma auwawa

Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza, Kitivo cha Sayansi ya Jamii katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Fredrick Joseph (25), ameuawa kwa kushambuliwa kwa kipigo na watu wanaosadikiwa kuwa ni wanafunzi wenzake wakati akitoka klabu ya pombe (Bar).


Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 25

RIWAYA: A WIZARD STUDENT (MWANAFUNZI MCHAWI)
MTUNZI:ENEA FAIDY
SEHEMU YA 25
..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.
"Vipi mke wangu?"
Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 24

RIWAYA: A WIZARD STUDENT ( MWANAFUNZI MCHAWI)
MTUNZI: ENEA FAIDY
SEHEMU YA 24
..Baada ya kutazama kioo cha simu Mr Alloyce alishtuka kidogo baada ya kukuta namba ya shemeji yake. Aliitazama kwa muda, huku akitafakari jibu la kumpa shemeji yake kwani tayari alimtaarifu kwamba aje kesho yake asubuhi. Aliamua kupokea simu ile huku akivuta pumzi ndefu na kuishusha taratibu sana. 
Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 23

RIWAYA: A WIZARD STUDENT ( MWANAFUNZI MCHAWI)
MTUNZI ENEA FAIDY

SEHEMU YA 23

...MR ALOYCE alolishikilia karatasi lile akiwa ameinamisha kichwa chake chini, mawazo yalimjaa tele kichwani mwake. Aliwaza achague lipi kati ya
Read More...