About KABENDE.COM

Manual Description Here: Ea eam labores imperdiet, apeirian democritum ei nam, doming neglegentur ad vis.

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 35

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 35
Mtunzi:Enea Faidy
......OOH siamini! Siamini kabisa kama sioni nyeti za Eddy" alisema Doreen akiwa amechanganyikiwa sana. Alitazama vizuri kwenye mkoba wake lakini hakuona nyeti za Eddy na hakujua nani amechukua. Kutokana na ulinzi mkali aliokuwa ameuweka ili kulinda vitu vile hakutaka kuamini kama Kweli vimeibiwa.
Doreen alikaa kitandani huku akifikiria kwa muda ndani ya chumba kile cha hoteli. Mawazo yake kila yalipofurika kichwani mwake,jasho jembamba lilimtiririka kwa kasi. "Mbona sielewi hii hali?" Alijiwazia huku akijaribu kutafuta tena nyeti zile ambazo kwake zilikuwa na thamani kubwa kuliko lulu. Doreen alikaa chini kwenye sakafu huku mawazo yakizidi kumuelemea.
Akavua nguo zote kisha akachukua mkoba wake na kuchukua kioo kidogo, akakipaka dawa ya ungaunga kisha akaanza kuomba dua kwa mizimu yake ili iweze kumsaidia katika janga lile gumu lililomkumba. "Mzimu wa Ngotongoto uliomkubwa sana katika ukoo wetu, Mtukufu Tatile na mizimu yako...
Tazama nilivyohangaika na kutafuta zawadi kubwa kama nilivyoagizwa lakini Leo hii sijui ni mzimu gani uliotokea na kutaka kunyang'anya kitu cha thamani kuliko dhahabu... Kafara iliyonzuri kwa mkuu wangu... Nihurumieni mja wenu! Naomba msaada wenu tafadhali.." Doreen alisema maneno Yale kwa hisia Kali huku akiwa ameinamisha kichwa chake chini na mikono yake ikiwa imeshikilia kioo kile. " Ee mizimu yangu tukufu... Nisaidie kumjua mwizi wangu ili nimshughulikie..."
Alisema Doreen na ghafla radi Kali ikapiga kwenye kioo kisha kioo chote kikatapakaa damu. Doreen alishtuka sana akaona hali si shwari maana kioo kile kutapakaa damu kilikuwa na maana ya uwepo wa vita Kali dhidi yake. Hofu ikamtawala sana binti yule, hofu ikamtanda akashindwa kuelewa ni nani adui yake haswaa!. "Doreen! Doreen! Inakubidi kupambana!" Ilisikika sauti nzito yenye mwangwi mkali lakini mzungumzaji hakuonekana. "Doreen! Tumia nguvu zako zote ulizonazo, sisi tuko nyuma yako...
Onesha uwezo wako ili uutwae utukufu.. Uwe malkia uliyetukukaaa!!" Iliisisitiza sauti ile iliyoongea kwa msisitizo wa hali ya juu. Doreen aliogopa sana, akajua tayari mwisho wake umewadia lakini hakuwa na budi kujipa moyo wa ushindi na kuwa na matumaini ya kumbaini mbaya wake. "Nani mpinzani wanguuuu? Nasema nani atampinga Doreen Mbwana mtoto wa kitanga? Kama yupo ajeee!" Alisema Doreen kwa ujasiri wa hali ya juu na kuivua hofu yote aliyokuwa nayo.
Ghafla upepo mkali ukavuma kwa nguvu ndani ya chumba kile cha hoteli. Sauti Kali ya kicheko kilichojaa dharau na jeuri ikasikika na kumfanya Doreen ahamaki sana. Hali ya taharuki ikazuka moyoni mwa Doreen kwani daima hakufikiria kutokewa na mpinzani wa kumpinga mambo yake. "Doreen! Wakati wako umekwisha! Uchawi wako na mateso yako kwa wanadamu wasio na hatia sasa umefika kikomo... Ha ha ha nakwambia Doreen huna nafasi tena!"
Ilisikika sauti nyembamba na nyororo ikimwambia Doreen. Doreen alishtuka sana kusikia maneno Yale. Kilichomtisha zaidi ni kwamba alishindwa kumuona mtu aliyezungumza. "Kama una uwezo njoo nikuone!" Alisema Doreen. "Ha ha ha! Nitakuja unione wala usiwaze" maneno Yale yalizidi kumchanganya Doreen alibaki kimya akiwa ametumbua mimacho kama vitunguu huku akitazama huku na kule ndani ya chumba lakini bado hakufanikiwa kumuona mtu yule aliyezungumza kwa dharau sana.
"Naongea na huyu binti nilimfananisha na Dorice" alisema mama Dorice na kuwafanya majirani zake wageuke kumtazama Kwa mshangao. Hakujua watu wale wanashangaa nini lakini kilichowashangaza ni kwamba walimsikia mama Dorice akizungumza lakini hawakujua anaongea na nani kwani hawakumuona yule mtu. "Dada upo sawa?" "Nipo sawa ndio! Kwani vipi?" "Muda mrefu sana unaongea peke yako hapa..." "We Majaliwa tuheshimiane....
Nitaongeaje peke yangu kwani Mimi mwehu?" Alisema Mama Dorice kwa ukali kiasi. Abiria ndani ya gari ile walimshangaa sana mama Doreen wakahisi labda hayupo sawa kiakili kwani jirani yake kwenye siti hakuwa mwanamke Bali ni mwanaume mtu mzima mwenye umri kama miaka arobaini na tano.
Na kwa muda wote aliokuwa akizungumza Mama Dorice mwanaume yule alilala usingizi. "Dada hebu mtazame jirani yako vizuri" alisema Majaliwa. Mama Doreen alitamtazama jirani yake kwa makini sana. Ghafla akapatwa na mshtuko wa ghafla Baada ya kuona aliyedhani ni binti anayeendana sana na mwanaye si mwenye siti ile.
Aliyekaa pale ni mtu mwingine tofauti. Mama Dorice alishtuka sana, moyo ukampasuka paah! Hakuamini macho yake. "Kaka Majaliwa!" "Naam dada!" "Mbona sielewi Mimi? Ni mtihani gani huu?" "Labda una malaria dada?" "Sina chochote ila nilikuwa nimekaa na binti Fulani hapa. ." "Mmh! Hapo pagumu.." Mama Dorice alishindwa kuelewa chanzo cha yote hayo ikabidi akae kimya tu.
Macho yake yakatua dirishani na kutulia kwa muda kama aliyetazama kitu kilichomvutia sana. Ghafla akamwona Dorice dirishani( dirisha la gari) akimpungia mkono wa kumuaga kisha akaachia busu la mbali la upendo. Mama Dorice alishtuka sana akabaki ameduwaa tu mpaka Dorice alipopotea ghafla. "Kaka!" Aliita......
ITAENDELEA.....
Read More...

RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 34

RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi - (A Wizard Student) - Sehemu ya 34
Mtunzi:Enea Faidy
...Lakini cha ajabu kila alipomsogelea binti yule naye alikaza mwendo zaidi. Mama Dorice alishuhudia jinsi ambavyo mwanaye alitembea kwa madaha sana.
"Doriiiice!" Aliita kwa sauti lakini yule msichana alipogeuka hakuwa Dorice tena ilikuwa ni sura ya msichana mwingine kabisa. Mama Dorice alichanganyikiwa sana, ni kwanini hali inakuwa vile? Lakini hakupata jibu. Kaka yake alimfata haraka na kumshika mkono.
"Dada utagongwa na magari... Kwani unamfata nani?" Aliuliza kwa mshangao kwani yeye hakumwona MTU yeyote.
"Namfuata Dorice..."
"Huyo Dorice yuko wapi maana tangu tupo kule unamfuata tu?"
"Sio yeye.. Nimemfananisha...."
"Dada bwana usiwaze sana.... Ona sasa mpaka watu wanakushangaa ujue.. Unaita kila mtu Dorice..."
"Lakini Mimi nilimwona kabisa kaka...."
"Haya tuondoke"
Mama Dorice alikuwa bado anaifikiria ile hali, akajua lazima kuna kitu kinaebdelea kuhusu Dorice, kwanini amfananishe kiasi kile lakini bado hakuwa na jibu sahihi.
Wakati wa safari ulipowadia, waliingia kwenye basi na kukaa kwenye siti zao.Walisafiri kwa mwendo kidogo, ndipo macho ya mams Dorice yalipotua kwenye sura ya yule binti aliyemwona toka wakiwa kituo cha mabasi Jana yake. Na alikuwa amevaa nguo zile zile, alikaa Pembeni yake. Moyo ulimpasuka kwa mshtuko akafikinya macho yake na kumtazama tena binti yule aliyeachia tabasamu mwanana. Akamsalimu mama Dorice. Mama Dorice alishangaa, kilichomshangaza zaidi ni kwamba alipoingia kwenye gari hakumwona MTU yule na hata alipokaa hakukaa na binti yule. Sasa imekuaje yupo nae?
"Mama nilikuona sehemu!"
"Mh hata Mimi nilikuona!" Alisema mama Dorice.
"Kwanini ulikuwa unanifata?" Aliuliza binti yule ambaye kila wakati alipenda kutabasamu.
"Nilikuwa na kufananisha na mwanangu" alisema mama Dorice.
"Mwanao? Anaitwa Dorice?"
"Ndio... Umemjuaje?"aliuliza mama Dorice lakini msichana yule alicheka sana kitendo kilichomshangaza mama Dorice.
"Mama we si uliniita Dorice?"
"Eeh ndo jina lake.." Wakati wakiendelea na mazungumzo Yale mjomba wake Dorice alimshangaa sana dada yake.
"Dada mbona unaongea peke yako? Unajibizana na nani?"
******
Mama Pamela alimtazama binti yake na kumsikiliza kwa umakini.
"Niliota nipo hapa sebuleni... Halafu nikakuona wewe ukiwa haujavaa nguo... Ukanifata na kunishika kifuani kwa muda kisha ukaniachia.... Halafu ulikuwa unatisha sana usoni...." Alisema Pamela.
Mama Pamela hakutaka kuamini kile alichokisikia, alipigwa na butwaa sana na kubaki kinywa wazi akimshangaa mwanaye.
"Mimi? Pamela! Mbona sikuelewi?"
"Ndio mama nilikuona wewe ukichukua titi langu.. Mama kwanini umenifanyia hivyo?" Pamela alisema kwa msisitizo huku akilia. Mama Pamela alizidi kuchanganyikiwa maana hakutegemea kusikia maneno Yale kutoka kwa mwanaye.
"Ina maana unataka kusema mimi ni mchawi? Pamela kweli unanisingizia hivyo?" Mama Pamela alikuwa haamini lakini hivyo ndivyo Pamela alivyoota. Kwani wakati Doreen akichukua titi lake, pamela hakuiona sura ya Doreen ila alions sura ya Mama yake hivyo aliamini kuwa mama yake ndiye aliyemfanyia vile.
"Mama! Sikujua kuwa wewe ni mchawi! Kumbe ndivyo ulivyo? Nilikuamini sana mama yangu... Kwanini umenifanyia hivi? Kwanini mama?" Alilalama Doreen na kuonesha ni jinsi gani alivyopoteza uaminifu tena kwa mama yake. Ilikuwa vigumu sana kwa Mama Pamela kumuamisha mwanaye kuwa sio yeye aliyefanya kitendo kile cha ukatili.
"Pamela mwanangu... Wewe ndo mwanangu wa pekee, sina mtoto mwingine zaidi yako Leo hii mimi nikufanyie hivyo? Haiwezekani..." Alijitetea mama Pamela.
"Lakini mama... Ili yote yaishe lazima unirudishie titi langu... Na usipofanya hivyo nampigia simu baba namwambia kila kitu.... Na sio baba tu nawaambia ukoo mzima..."
"Pamela... Sio mimi mwanangu... Nisemeje unielewe?" Mama Pamela alijitahidi kujitetea kadri awezavyo lakini bado ilikuwa vigumu kueleweka. Pamela alilia sana huku akimbebesha mama yake mzigo wa lawama. Alichukua simu na kumpigia baba yake, hofu ikamvaa mama Pamela akiifikiria aibu kubwa ambayo angeipata kwenye ukoo wake na wa mumewe. Mpaka muda ule hakujua kinachoendelea kwa Doreen, kwani alidhani yupo chumbani kwake bila kujua Doreen alishaondoka muda mrefu. Kibaya zaidi kilichompa hofu ni kwamba mumewe angeamini maneno ya Pamela kutokana na jinsi mama Pamela alivyokuwa akimtetea Doreen.
"Lazima aamini... Na atajua ni kweli nimefanya hivyo ndio maana nilimkatalia sana Doreen... Haya majanga ya kupewa uchawi wakati mimi so mchawi!" Aliwaza mama Pamela bila kujua hatma ya tatizo lile.
"Daddy!" Alisema Pamela baada ya simu kupokelewa.
"Yes Pamela... Eti nini kimekupata mwanangu...?" Aliuliza Baba Pamela. Pamela akaongeza kilio huku akimtazama mama yake.
"Daddy! Fanya haraka uje... Kuna mambo mazito sana baba.. " alisema Pamela.
"Nakuja Leo jioni na ndege...."
"Uje tu baba yangu... Uje haraka.." Alisema Pamela huku akishindwa kuyazuia machozi yake.
Mama yake alibaki kimya huku machozi yakimdondoka. Alishindwa afanyeje.
"Unalia nini na huo uchawi wako?" Alisema Pamela kwa hasira huk
Oy...
ITAENDELEA.....
Read More...