RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 25

RIWAYA: A WIZARD STUDENT (MWANAFUNZI MCHAWI)
MTUNZI:ENEA FAIDY
SEHEMU YA 25
..DORICE alimshangaa Mumewe Mansoor kwa maneno yake. Machozi yalimlengalenga machoni mwake kisha akajiondoa kifuani kwa Mansoor na kujitenga kando.
"Vipi mke wangu?"
"Najuta Mansoor.. Najuta sana kukukubalia, sikujua kama hautakuwa mwaminifu kwa ahadi zako!" Alisema Dorice kwa hasira.
"Sina maana mbaya mke wangu mpenzi.. Usinielewe vibaya tafadhali...Nakupenda sana!"
"Unanipenda? Unanipenda nini uongo mtupu..!" Alisema Dorice kwa hasira huku machozi yakimshuka mashavuni mwake. Alijikuta anamchukia Mansoor kupita kiasi. Hakutaka hata kumsogelea karibu.
"Baby! Nimekuelewa basi naomba uwe na amani moyoni mwako" alisema Mansoor huku akimsogelea Dorice na kutaka kumkumbatia lakini Dorice alimsukumia kando Mansoor na kuongeza kilio chake.
"Sitaki uniguse mpaka utakaponiambia ni lini utatimiza ahadi yako"
"Baada ya wiki moja nitaitimiza ahadi yako..!" Alisema Mansoor kwa huzuni kwani alijua ni kiasi gani Dorice alimpenda Eddy na alijua kwamba endapo angemrudisha Dorice duniani basi angemsahau Yeye na kuponda raha na Eddy. Kila alipofikiria hilo Mansoor aliumia sana moyoni mwake. Hakutamani kumkosa Dorice lakini hakuwa na jinsi zaidi ya kutunza uaminifu wa kutimiza ahadi yake.
"Una uhakika utanipeleka baada ya wiki moja?" Aliuliza Dorice akimtazama Mansoor.
"Ndio.. Usijali!" Mansoor alijibu kwa unyonge sana.
"Hapo umenifurahisha!" Alisema Dorice na kumkumbatia Mansoor.
"Lakini kabla haujaenda huko kuna kitu muhimu unatakiwa ufanye!" Alisema Mansoor akiwa bado amemkumbatia Doreen.
"Kitu gani?" Aliuliza Dorice.
Mansoor alimuachia Dorice kisha akanyoosha mkono wake na kumuonesha Dorice kiganja cha mkono wake. Kwa mshangao kidogo, Dorice akatazama kiganja cha Mansoor.
"Unaona nini hapa?"
"Sioni kitu.."
"Huoni kitu? Hebu tazama vizuri"
"Naona Pete" alijibu Dorice kwa mshangao.
*********
Eddy alimtazama kwa mshangao mlinzi wao. Alimkazia macho huku akimwomba msamaha kwa kumjibu vibaya hapo mwanzo.
"Usijali.. Najua matatizo yako yanakufanya uwe hivyo" alisema mlinzi.
"Sasa utanisaidiaje? Maana nateseka sana!"
"Nitakusaidia tu wala usiwe na haraka... "
"Lazima niwe na haraka Anko maana mpaka sasa hivi sijawahi hata kukojoa!"
"Mmh! Haraka zilimponza chura zikafanya awe na mabaka. Vuta subira tu maana umefanyiwa mchezo mbaya sana." Alisema mlinzi yule huku akijifunika vyema shuka lake na kujigesha ukutani ili amalizie usingizi wake. Lakini ghafla akapigwa Kofi zito shavuni, aliruka kama kuku aliyeona hatari. Kabla hajakaa sawa Kofi lingine zito lilitua shavuni kwake, akajishika shavu na kutazama kama alikuwa amechanika lakini haikuwa hivyo kwani hakukuwa na damu yoyote ile.
Mlinzi yule akatazama huku na kule lakini hakuona Mtu aliyempiga makofi Yale mazito yaliyotua shavuni kama radi wakati wa mvya Kali.
"Vipi Anko?"
"Ah.. Hanna kitu.. Niko sawa tu.."
"Mbona umeruka sana?"
"Usijali Eddy.. Mimi nimeaga kwetu Musoma.. Niliwaaga wajita wenzangu..!" Alisema Mlinzi huku akisikilizia maumivu makali ya vibao alivyopigwa.
"Sikuelewi Anko ."
"Nimeaga.. Hakuna wa kunichezea!" Alizidi kuropoka mlinzi yule kisha akatulia kimya. Mawazo tele yakamjaa kuhusu vibao vile alivyopigwa kiuchawi. Aliwaza sana kwani alikuwa ana zindiko kubwa sana, sasa kwanini apigwe vile wakati ana kings anayoiamini? Alijiuliza sana bila kupata jibu.
Kulipambazuka kabisa, kimwanga kidogo cha jua kilianza kuchomoza kwa mbali. Wakati huo Mr Alloyce alikuwa kwenye gari take kuelekea msituni alikopotelea Mama Eddy.
Kichwani mwake alifikiria sana jinsi ya kutatua matatizo yanayoikumba familia yake. Hakupata njia kamili ya kuweza kutatua matatizo yake.
Aliendesha gari kwa mwendo wa SAA moja na nusu hatimaye akawasili kwenye eneo alilotakiwa kufika, akashuka kwenye gari na kuangaza macho yake huku na kule kuona kama atamwona mkewe.
******
"Amka mama Pamela kuna jambo nataka nikuambie"
"Bwana utaniambia asubuhi"
"Huu ndo muda mzuri wa kukuambia lakini kama hutaki basi.. " Alisema baba Pamela kwa sauti ya utulivu sana . Licha ya ubishi aliokuwa nao mama Pamela katika suala la kuamka lakini ilimbidi tu aamke ili amsikilize mume wake. Kwani alijua huenda ana jambo muhimu anataka kumueleza wakati ule.
"Niambie basi mume wangu!" Alisema mama Pamela huku akipiga miayo ya uchovu wa usingizi.
"Asubuhi ya Leo nina safari kikazi.."
"Unaenda wapi?" Aliuliza mama Pamela.
"Naenda Arusha mke wangu... Nilitemea nikuambie Jana ila uliniudhi mpaka nikashindwa kukuambia"
"Mmh! Utakaa muda gani?"
"Mwezi mmoja!"
"Mwezi mzima? Mbona mrefu hivyo?"
"Ndio hivyo mke wangu ni masuala ya kazi tu, sina jinsi"
"Imekuwa ghafla!"
"Ndio nimepewa taarifa juzi jioni, lakini...."
"Lakini nini?" Alishtuka mama Pamela
"Nikiondoka tu, na huyo mgeni wako atoke hapa nyumbani kwangu"
Alisema Baba Pamela kwa sauti ya msisitizo sana akidhihirisha kuwa alimaanisha kile alichokisema.
"Baba Pamela utaniudhi.. Sitaki maudhi yako na hiyo roho mbaya yako"
"IPO siku utafahamu kwanini nasema hivo.. Kaa vizuri na Mungu utafahamu mengi!" Alisema Baba Pamela kisha akajifunika vizuri na kulala ili aamke baada ya nusu saa.
Mama Pamela alibaki na mawazo mengi sana ila katu hakuwa tayari kumwacha Doreen aende zake. Alimwonea huruma binti yule kwani alishamwambia historian nzima ya maisha yake.' Mime wangu sijui yukoje siku hizi.. Ana roho mbaya.. Simfukuzi ng'oo Doreen. Mtoto ana adabu tena mstaarabu' aliwaza Bi Carolina.
Asubuhi na Mapema Baba Pamela alijiandaa na kuwahi uwanja wa ndege, Bi Carolina alimsindikiza mumewe hadi uwanja wa Songwe Airport Kisha akamuaga.
"Ila tekeleza nilichokuambia"
"Sawa !" Alijibu Bi Carolina kisha akaingia kwenye gari na kuondoa gari kuelekea nyumbani kwake.
Haukupita muda mrefu Bi Carolina alitia timu nyimbani kwake, akapaki gari na kuingia ndani. Lakini alipoingia ndani alikutana na hali ya utofauti.
ITAENDELEA
LIKE, COMMENT , SHARE

1 Response to "RIWAYA YA MWANAFUNZI MCHAWI SEHEMU YA 25"

  1. Casino - Mapyro
    › 2021/04/10 › 안동 출장안마 casino-casinor › 2021/04/10 영천 출장샵 › casino-casinor 경상북도 출장안마 Casino is a fun and exciting place to play your favorite 동해 출장마사지 games. Play online games 광주광역 출장마사지 for free in demo mode.

    ReplyDelete